HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, July 23, 2017

TRA YAKABIDHI MSAADA WA VIFAA MBALIMBALI KATIKA KITUO CHA AFYA MAGOMENI

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
MAMLAKA ya Mapato Nchini (TRA ) imetoa msaada  vifaa mbambali katika kituo cha afya cha Magomeni  ambavyo vilitelekezwa  kutokana na kodi.

Akikabidhi msaada huo, Meneja wa Huduma wa Elimu ya Mlipakodi, Valentina Baltazar amesema kuwa kutokana na sheria Kamishina Mkuu ana mamlaka ya kutoa vitu vilivyotelekezwa kwa ajili ya kusaidia jamii .

Amesema vifaa hivyo vina zaidi ya miaka mitano  vipo  katika ghala ya  ubungo  vikiwa vimetelekezwa kutokana na kushindwa  kulipiwa  kodi  na mtu aliyekuwa ameviagiza.

Valentina amesema kuwa Kituo cha Afya  Magomeni waliomba vifaa hivyo katika mamlaka  na kujiridhisha na maombi ya kutoa  vifaa hivyo kwa ajili  kusaidia wananchi.

Nae Mganga Mfawidhi  wa Kituo cha Afya Magomeni ,Dk. Faith Mdee amesema kuwa msaada huo ni mkubwa sana ambao utakwenda kusaidia hata hospitali ya Mwananyamala.

Amesema baada ya kupoke vifaa hivyo sasa changamoto iliyobaki kwao ni gari la kubeba wagonjwa ambapo wameoimba TRA kama wa  magari waweze kuwasiadia.
Meneja wa Huduma wa Elimu ya Mlipakodi wa TRA, Valentina Baltazar akizungumza na waandishi habari mara baada ya kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali katika Kituo cha Afya cha Magomeni.
Mganga Mfawidhi  wa Kituo cha Afya Magomeni ,Dk. Faith Mdee akizungumza na waandishi habari juu ya msaada katika kituo cha afya cha Magomeni.
Meneja wa Huduma wa Elimu ya Mlipakodi wa TRA, Valentina Baltazar akimkabidhi  moja kitanda cha wagonjwa kwa Muuguzi Mfawidhi  wa Kituo cha Afya Magomeni , Upendo Mkuluma  jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya  nguo mbalimbali za msaada katika Kituo cha Afya Magomeni.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad