HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, July 27, 2017

SEKRETARIETI YA KITAIFA YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA BIASHARA HARAMU YA USAFIRISHAJI BINADAMU WAKUTANA JIJINI DAR ES SALAAM.

 Katibu wa Kamati ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu,Seperatus Fella, akizungumza kwenye Kikao kilichowakutanisha    wajumbe wa Kamati na Sekretarieti ya Kitaifa ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu,lengo ikiwa ni kupitia Sheria inayohusu   biashara hiyo.Wengine ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo,Adatus Magere na Mkurugenzi wa Mradi wa kuzuia biashara hiyo kutoka Taasisi ya Kimataifa ya RTI, Dk. Lyungai Mbilinyi.Kikao hicho  kimefanyika leo katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi,jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
 Mkurugenzi wa  Mradi wa Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu kutoka Taasisi ya Kimataifa ya RTI, Dk. Lyungai Mbilinyi, akizungumza kwenye kikao   kilichowakutanisha wajumbe wa Kamati na Sekretarieti ya Kitaifa ya Kuzuia na Kupambana na Biashara hiyo,lengo ikiwa ni kupitia Sheria  zinazosimamia biashara hiyo.Wengine ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo,Adatus Magere na Katibu wa Kamati ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu, Seperatus Fella. Kikao hicho kimefanyika  leo katika  Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi,jijini Dar es Salaam.
 Mjumbe wa Kamati na Sekretarieti ya Kitaifa ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu,Hamad Mwe-ndadi, akizungumza wakati wa Kikao  chakupitia Sheria  inayosimamia biashara hiyo.Kikao hicho kimefanyika  leo katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi,jijini Dar es Salaam. 
 Mmoja kati ya wajumbe wa Kamati na Sekretarieti ya Kitaifa ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu, akizungumza wakati wa Kikao cha kupitia Sheria   inayosimamia biashara hiyo. Kikao hicho  kimefanyika leo katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi,jijini Dar es Salaam. 
Wajumbe  wa Kamati na Sekretarieti ya Kitaifa ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu,wakiwa katika majadiliano  wakati wa Kikao cha  kupitia Sheria  inayosimamia biashara hiyo. Kikao hicho   kimefanyika leo katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi,jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad