HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, July 11, 2017

MSTAAFU ATOA WITO WANANCHI KUJIUNGA NA PSPF KUPITIA UCHANGIAJI WA HIARI PSS, ASEMA AMEONA FAIDA ZAKE IKIWEMO BIMA YA AFYA

Mwanachama mpya wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, kupitia Uchangiaji wa Hiari, (PSS), Bi. Sania M.Noor, akionyesha kadi yake ya uanachama baada ya kujiunga leo Julai 10, 2017, alipotembeela banda la Mfuko huo, lililoko jengo la Wizara ya Fedha na Mipango, kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam, ambako kunafanyika maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

MSTAAFU wa utumishi wa umma, Bi. Marcella Isidori Chanda, amewahimiza wananchi na wastaafu wenzake, kujiunga na Mfuko wa Pensehni wa PSPF, kupitia mpango wake wa uchangiaji wa Hiari, (PSS), kwani kuna faida nyingi mwanachama atazipata.

Bi. Chanda, ameyasema hayo muda mfupi baada ya kujiunga na Mpango huo wa PSS, leo Julai 10, 2017, baada ya kupatiwa elimu ya huduma zitolewazo na PSPF kwa wanachama wake.

“Mimi nilikuwa mtumishi wa benki na nimestafu mwaka 2013, ni meona iko haja ya kujiunga na mpango huu ambao hatimaye moja ya mambo yaliyonivutia ni kupatiwa bima ya afya, kwani nimeelzwakuwa ukiwa mwanachama wa PSS, basi unapata sifa za kujiunga na bima ya Afya, tofauti na ukiwa mtu binafsi gharama zinakuwa kubwa mno na zinafikia hadi shilingi 1,500,000nkwa mwaka.” Alisema Bi. Chanda.

Akieleza zaidi, Bi. Chanda alisema, amefikia uamuzi wa kujiunga naPSPF, baada ya kupata taarifa nyingi kupitia vyombo vya habari kuwa, lakini pia majirani na jamaa zngu kuwa wamekuwa wakifaidika na huduma ya afya kupitia bima ya afya.

Mstaafu huyo alsiema, leo amejiunga na PSS na pia atamueleza mumewe naye pia ajiunge. “Natoa wito wka wastaafu wenzangu na wananchi kwa ujumla kujiunga na PSPF ili kujihami na gharama za matibabu. Kwa upande wake, Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Abdul Njaidi alisema, karibu asilimia 60 ya wananchi wanaofika kwenye banda hilo, wamekuwa wakijunga na Mpango wa PSS na moja ya sababu kubwa ni kupatiwa bima ya Afya.

Mwananchi akijaza fomu kujiunga na PSS.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani, (kulia), akizungumza jambo mbele ya Afsia Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Abdul Njaidi alipotembelea banda la Mfuko huo leo Julai 10, 2017.

Mkurugenzi wa Mawasiliano na Elimu kwa Umma, wa Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi Hifadhi ya Jamii, (SSRA), Bi. Sarah Kibonde Msika, (kushoto) akimsikiliza Bw. Njaidi kwenye banda la PSPF, Julai 10, 2017. SSRA imeweka maafisa wake katika kila banda la Mifuko ya Hifadhio ya Jamii, ili kufuatilia utoaji huduma wa Mifuko hiyo kwa wananchi kwenye maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa huduma za Habari na Utangazaji wa Mamlaka ya Utangaza Tanzania, (TCRA), Bw. Freddyb Ntobi, (kulia), aimskiliza Bw. Njaidi alipotembeela banda la Mfuko huo.

Afasia Msaidizi wa Uenddshaji wa PSPF, Bw. Win-God Simon, (kushoto), akiwahudumia maafisa hawa wa polisi ambao ni wanachama wa Mfuko.


Mama huyu (kushoto), akiuliza kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na PSPF alipotembelea banda la Mfuko huo leo Julai 10, 2017.

Afisa Uendeshaji wa PSPF, Bi. Irine Musetti, (kushoto), Afisa Mkuu wa TEHAMA wa Mfuko huo, Bi. Mariam Saleh, (katikati), na Afisa wa Sheria wa SSRA, Bi.Imani Masebu, wakijadiliana jambo kwenye banda la PSPF.

Bereket S. Singili, (kushoto), akiangalia jinsi Afsia huyu wa PSPF, anavyomjazia fomu ya kujiunga na Mfuko huo kupitia PSS.

Bw. Singili, (kushoto), akikabidhiwa kadi yake ya uanachama na Afisa wa Fedha wa PSPF, Bw.Msina.

Mhandis Ali Shanjirwa, (kushoto), wa Mfuko wa Pensehni wa PSPF, akimuhudumia mwananchi huyu aliyefika kwenye banda la Mfuko huo ili kupatiwa huduma.

Afisa Uendeshaji wa PSPF, Bw. Noah, (kushoto), akitoa huduma kwa wananchi hawa waliofika banda la PSPF leo Julai 10, 2017.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad