HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, July 30, 2017

MANTRACK TANZANIA YAONESHA MAPINDUZI MAPYA YA TEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA UJENZI NCHINI

Katika kuunga juhudi za Serikali ya awamu ya tano ya kuleta maendeleo kwa wananchi kampuni ya magari ya Mantrack Tanzania jana imeendesha warsha fupi yenye lengo la kutambulisha vifaa na teknolojia mpya itakayoongeza ufanisi wa kazi hasa katika sekta ya ujenzi.

Akizungumza na waandishi wa habari, mwakilishi wa kampuni ya Mantrack Tanzania alisema kuwa wameleta vifaa vipya vitakavyoendana na kasi ya maendeleo ya Serikali ya awamu ya tano ya kuhakikisha Tanzania mpya inajengwa na uchumi bora na yenye miundombinu bora.

“Vifaa hivi ni imara na vinatumia teknolojia mpya na ya kisasa inayosaidia utendakaji wa shughuli za ujenzi kuwa rahisi. Tumeamua kuja na kasi ya serikali mpya ya kutenda vitu kwa urahisi na kwa ufanisi wa hali ya juu”.

Tuna wakaribisha wadau wa ujenzi wafike kujionea wenye tunachosema. Alisema. Warsha hiyo imefanyika katika karakana ya Mantrack Tanzania iliyopo karibu na jengo la Quality Plaza barabara ya Nyerere na ilihudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka makampuni mbalimbali ya ujenzi hapa nchini waliofika kushuhudia vifaa hivyo vinavyofanya kazi.
Mwakilishi wa ManTrack Tanzania akitoa maelezo mbalimbali kwa wadau juu ya teknolojia mpya na bidhaa zao mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad