HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 7, 2017

BEN POL AFURAHISHWA NA UJIO WA MSANII WA MUZIKI WA KIASILI SAIDA KAROLI

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MSANII wa muziki wa kizazi kipya Benard Paul 'Ben Pol' amesema amefurahishwa sana na kurejea kwa mwanamuziki wa mziki wa asili Saida Karoli kwani bado ana uwezo mkubwa wa kuimba.

Ben Pol amesema hayo wakati wa tamasha maalumu lililoandaliwa kwa ajili ya kurejea kwa mwanamuziki huyo aliyetamba zamani na nyimbo zenye asili ya kihaya ikiwa ni miaka 15 toka aanze muziki.

Tamasha la Rise and Fall ya Saida Karoli iliyofanyika jana usiku kwenye fukwe za EScape One na lilikutanisha wasanii mbalimbali na viongozi waliojitokeza kumuunga mkono mwanamama huyo ambaye alipotea kimuziki kwa kipindi kirefu.

Amesema kuwa, Saida bado ana uwezo mkubwa sana wa kimuziki na hilo amelithibisha pale alipotoa wimbo wake mpya na watanzania kuukabali kwa asilimia zote na ameendelea kuonyesha uwezo wake katika kuimba.

"Namkubali sana Saida kwani ni mwanamuziki mzuri na ameonyesha uwezo mkubwa katika tasnia ya muziki na amerejea kwa nguvu kubwa sana na nyimbo yake imekubalika,"amesmea Ben Pol.


Saida ametoa wimbo wake mpya ujulikanao kama Urugambo ulio katika mahadhi ya kihaya na umeonekana kushika kasi sana.

Mbali na hilo, Ben Pol aliambatana na msanii wa vichekesho anayejulikana kama Ebitokea ambapo kwa sasa wanahisiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi.

Kwa upande wa Ebitoke alisema kuwa anafurahi sana kuwa na Ben Pol na anafarijika sana kwani 
Msanii Ben Pol akiwa katika picha ya pamoja na msanii wa vichekesho Ebitoke katika Tamasha la Rise and Fall ya Saida Karoli iliyofanyika jana usiku kwenye fukwe za EScape One.

Msanii wa Vichekesho Ebitoke akizungumzia mahusiano yake na Ben Pol.
Msanii Ben Pol akizungumzia ujio mpya wa msanii wa muziki wa kiasili Saida Karoli katika Tamasha la Rise and Fall ya Saida Karoli iliyofanyika jana usiku kwenye fukwe za EScape One.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad