HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, June 11, 2017

WAKAAZI WA MBEZI BEACH NA MIKOCHENI B JIJINI DAR ES SALAAM WASAFISHA FUKWE ZA BAHARI

 Mjumbe wa Serikali za Mtaa wa Mikocheni B, Kamati ya Mazingira Moses Sanga pamoja na Victoria Kileo wa Nipe Fagio wakiwa wamebeba taka wakati wa zoezi la kufanya usafi katika fukwe za Mbezi Beach leo Jijini Dar es Salaam. Zoezi hilo limeshirikisha Marafiki wa Bahari, Nipe Fagio,Mbezi Beach Neighborhoods. 
 Delicia Mwanyika and Cindy Tibazarwa kutoka Mbezi beach Neighborhoods wakishirikiana kuokota taka sugu kama vile Plastiki, makopo, nguo, viatu, nyavu, mataili, sindano, vyupa na taka nyinginezo.
 Beatrice Steyn Muasisi wa Mbezi Beach Neighborhoods akizungumza na waandishi wa habari wakati wa  zoezi la kufanya usafi wa fukwe ya Mbezi Beach katika kuokoa Bahari ambapo alisisitiza ushirikiano kutoka Serikali, Viwanda, Taasisi mbalimbali pamoja na watu binafsi kuungana kwa pamoja kurudisha uhai wa bahari ambayo inaelekea kufa kama hakuna hatua itakayo chukuliwa sasa.
 Boss Brown Muasisi wa Marafiki wa Bahari kutoka Mikocheni B akiwa katika zoezi la kufanya usafi katika fukwe za Mbezi Beach leo Jijini Dar es Salaam. Zoezi hilo limeshirikisha Marafiki wa Bahari, Nipe Fagio,Mbezi Beach Neighborhoods
Washiriki wa zoezi la usafi wa fukwe wa Mbezi Beach wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza kwa zoezi hilo leo Jijini Dar es Salaam. Zoezi hilo ni harakati za kuunga mkono kampeni ya kuiokoa Bahari ambalo limeshirikisha asasi za Nipe Fagio, Mbezi Beach na Friends Of Ocean kutoka Mikocheni B chini ya udhamini wa Nabaki Africa, Koncept Communication Pamoja na AFM 92.9 ya mjini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad