Mjumbe wa Serikali za Mtaa wa Mikocheni B,
Kamati ya Mazingira Moses Sanga pamoja na Victoria Kileo wa Nipe Fagio wakiwa
wamebeba taka wakati wa zoezi la kufanya usafi katika fukwe za Mbezi Beach leo
Jijini Dar es Salaam. Zoezi hilo limeshirikisha Marafiki wa Bahari, Nipe
Fagio,Mbezi Beach Neighborhoods.
Delicia Mwanyika and Cindy Tibazarwa kutoka
Mbezi beach Neighborhoods wakishirikiana kuokota taka sugu kama vile Plastiki,
makopo, nguo, viatu, nyavu, mataili, sindano, vyupa na taka nyinginezo.
Beatrice Steyn Muasisi wa Mbezi Beach
Neighborhoods akizungumza na waandishi wa habari wakati wa zoezi la kufanya usafi wa fukwe ya Mbezi Beach
katika kuokoa Bahari ambapo alisisitiza ushirikiano kutoka Serikali, Viwanda,
Taasisi mbalimbali pamoja na watu binafsi kuungana kwa pamoja kurudisha uhai wa
bahari ambayo inaelekea kufa kama hakuna hatua itakayo chukuliwa sasa.
Boss Brown Muasisi wa Marafiki wa Bahari kutoka
Mikocheni B akiwa katika zoezi la kufanya usafi katika fukwe za Mbezi Beach leo
Jijini Dar es Salaam. Zoezi hilo limeshirikisha Marafiki wa Bahari, Nipe
Fagio,Mbezi Beach Neighborhoods
Washiriki wa zoezi la usafi wa fukwe wa Mbezi
Beach wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza kwa zoezi hilo leo Jijini
Dar es Salaam. Zoezi
hilo
ni harakati za kuunga mkono kampeni ya kuiokoa Bahari ambalo limeshirikisha
asasi za Nipe Fagio, Mbezi Beach na Friends Of Ocean kutoka Mikocheni B chini
ya udhamini wa Nabaki Africa, Koncept Communication Pamoja na AFM 92.9 ya mjini
Dodoma.
No comments:
Post a Comment