HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, June 23, 2017

Swala ya eid El fitri kufanyika siku ya jumatatu viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar - Alhad Mussa Salum

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhad Mussa Salum amewatangazia waumini wa dini ya kiislam kuwa Swala ya eid El fitri itaswaliwa mnamo siku ya jumatatu Juni 26, 2017 katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam, ikiwa ni baada ya kukamilika mfungo mtukufu wa mwezi wa Ramadhani.

Sheikh Salum aliyazungumza hayo jana wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari, na amewataka na kuwaasa waumini wa kiislam kuhakikisha wanatekeleza mema yote kama waliyokuwa wakiyafanya katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Akizungumzia siku ya ibada hiyo muhimu kwa waislam wote ulimwenguni, Sheikh Salum alimesema katika viwanja vya mnazi wageni mbali mbali wanatarajiwa kuwepo, lakini pia mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaj Ali Hassan Mwinyi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad