HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, June 1, 2017

MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA MKOANI MBEYA...

Afisa Maliasili Mkoa wa Mbeya Ndugu, Joseph Butuyuyu akizungumza na globu ya jamii alipokuwa akizungumzia juu ya Maadhimisho ya kilele cha mazingira duniani yanayo tarajia kufanyika siku ya Tarehe 5,mwezi wa 6, mwaka huu Ambapo kimataifa yatafanyika Nchini Canada, Kitaifa yatafanyika Mkoani Mara na Kwa Mkoa wa Mbeya yanatarajiwa kufanyika wilayani mbarali katika eneo la mabadaga siku hiyo ya Juma Tatu na mgeni Rasmi kwa mkoa wa Mbeya Atakuwa ni mkuu wa mkoa wa mbeya Mh.Amos G. Makalla na watu wote Mnakaribishwa.

Ndugu, Joseph Butuyuyu Pia aliongeza kwa kuwataka wananchi wa mkoa wa mbeya kutunza na kuthamini mazingira yanayo wazunguka ili kupendezesha na kuyatunza vizuri mazingira ya mkoa wa mbeya na kuwataka wananchi kuchungamkia fursa ya kutembelea vivutio mbalimbali ikiwemo mbuga za wanyama bira kulipa kiingilio chochote kwa siku tatu mfululizo kuanzia siku ya Tarehe 2, mpaka Tarehe 4, ya mwezi huu.

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya Mazingira Duniani kwa mwaka huu ni   (Mausiano endelevu kati ya Binadamu na Mazingi) hiyo ikiwa ni kimataifa na kitaifa ni.. (Hifadhi ya Mazingira ni Muhimili kwa Tanzania ya Viwanda)
NA MR.PENGO MBEYA.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad