HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, June 30, 2017

DC MKURANGA AZINDUA JUKWAA LA UWEZESHAJI WANAWAKE WA WILAYA HIYO

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Filbert Sanga amewataka wanawake wa Wilaya hiyo kuachana na masuala ya utegemezi kwa wanaume na zaidi wajikite katika kujiendeleza kiuchumi kwa kuanzisha miradi midogo midogo ikiwemo kuanzisha vikundi vya ujasiriamali  ikiwa ni katika kutekeleza maagizo ya Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu ya kila Wilaya kuwa na vikundi vya kujiinua kiuchumi..

Amesema hayo wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la Uwezeshaji wanawake lililofanyika jana na kuvikutanisha zaidi ya vikundi 30 kutoka Wilaya ya Mkuranga na kuelezea matatizo wanayokumbana katika vikundi vyao.

Sanga amewaambia kuwa wanawake bila kuwezeshwa wanaweza wakajiendeleza wenyewe kwani utakapomuelimisha mwanamk mmoja utakuwa umeelimisha watu wnegi sana.

"wanawake mkijiwezesha wenyewe mnaweza sio lazima muwezeshwe kwani tunachoamini ni kuwa ukimuelimisha mwanamke umeelimisha dunia kwani nyinyi ndiyo msingi mkubwa wa familia katika jamii zinazotuzunguka mtakapoamua kukaa na kutokujishughulisha basi hakutakuwa na msingi mzuri wa kizazi kijacho,"amesem Sanga.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji  WanawakeWilaya ya Mkuranga Mariam Ulega alisema kuwa anashukuru sana kwa Mkuu wa Wilaya kuja kuwazindulia jukwaa lao na cha zaidi kwa kuwa wameshapatikana viongozi wa Jukwaa hilo kwa wilaya ya Mkuranga na zaidi anaomba umoja na ushirikiano kutoka kwa wakina mama kutoka kata mbalimbali ili kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa.

Kabla ya kuzinduliwa kwa jukwaa hilo ulifanyika uchaguzi na kupatikana kwa Mwenyekiti Mariam Ulega. 
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Filbert Sanga akizindua Jukwaa la Uwezeshaji wanawake lililofanyika jana na kuwasihi wanawake kuachana na masuala ya utegemezi zaidi wanatakiwa kujiendeleza ili kujiinua kiuchumi na pia kuviendeleza vikundi vyao na kuvisajili ikiwa ni katika kutekeleza maagizo ya Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu ya kila Wilaya kuwa na vikundi vya kujiinua kiuchumi.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Wilaya ya Mkuranga Mariam Ulega akizungumza na wakina mama wa wilaya hiyo kutoka kata mbalimbali kuhusiana na kuviendeleza vikundi vyao kwa ajili ya kuacha kuwa tegemezi kwa wanaume ikiwa ni katika kutekeleza maagizo ya Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu ya kila Wilaya kuwa na vikundi vya kujiinua kiuchumi.


 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Filbert Sanga akipokea maandamano ya wakina mama wa Mkuranga wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la Uwezeshaji wanawake lililofanyika jana na kuwasihi wanawake kuachana na masuala ya utegemezi zaidi wanatakiwa kujiendeleza ili kujiinua kiuchumi na pia kuviendeleza vikundi vyao na kuvisajili ikiwa ni katika kutekeleza maagizo ya Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu ya kila Wilaya kuwa na vikundi vya kujiinua kiuchumi.
 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Filbert Sanga  akisaini kitabu cha wageni wakati alivyowasili katika uzinduzi wa Jukwaa la Uwezeshaji wanawake lililofanyika jana na kuwasihi wanawake kuachana na masuala ya utegemezi zaidi wanatakiwa kujiendeleza ili kujiinua kiuchumi na pia kuviendeleza vikundi vyao na kuvisajili ikiwa ni katika kutekeleza maagizo ya Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu ya kila Wilaya kuwa na vikundi vya kujiinua kiuchumi.

  Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Filbert Sanga akioneshwa baadhi ya bidhaa zinazotengenezwa na wakina mama hao wa Wilaya ya Mkuranga kutoka katika Vikundi mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la Uwezeshaji wanawake lililofanyika jana na kuwasihi wanawake kuachana na masuala ya utegemezi zaidi wanatakiwa kujiendeleza ili kujiinua kiuchumi na pia kuviendeleza vikundi vyao na kuvisajili ikiwa ni katika kutekeleza maagizo ya Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu ya kila Wilaya kuwa na vikundi vya kujiinua kiuchumi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad