Makamu Mwenyekiti kutoka Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Radhimina Mbilinyi akifungua Semina ya uelimishaji kwa Waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi jijini Dar es Salaam leo.
Afisa Matekelezo Mwandamizi kutoka Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) akitoa mada katika semina ya uelimishaji kwa Waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt. Abdullssadaam Omary akitoa mada katika semina ya uelimishaji kwa waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya washiriki wa semina ya uelimishaji kwa waajiri wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wa semina hiyo ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Bi. Radhimina Mbilinyi jijini Dar es Salaam leo.
Afisa Matekelezo Mwandamizi kutoka Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) akitoa mada katika semina ya uelimishaji kwa Waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt. Abdullssadaam Omary akitoa mada katika semina ya uelimishaji kwa waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya washiriki wa semina ya uelimishaji kwa waajiri wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wa semina hiyo ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Bi. Radhimina Mbilinyi jijini Dar es Salaam leo.
Na Benjamin Sawe.
Mfuko wa
Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), umeendesha semina ya siku moja kwa waajiri nchini ili
kutoa elimu juu ya shughuli za Mfuko na wajibu wa waajiri kwa wafanyakazi wao
katika kujisajili na kuwalipa michango kwa niaba ya waajiriwa wao.
Akizungumza
katika semina hiyo Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko huo Radhimana Mbilinyi amesema
kuanzishwa kwa mfuko huo kumekuja wakati muafaka ambapo Tanzania inaelekea
katika uchumi wa viwanda hivyo kupelekea ongezeko la wafanyakazi ambapo chombo
hicho ndio mkombozi wa majanga yatokanayo na kazi.
“Ni muda
muafaka kwa waajiri kutambua wajibu wenu katika Mfuko huu na pia kutambua
madhara ya kutotekeleza wajibu wenu” Alisema Radhimina Mbilinyi.
Katika hotuba
yake, Bi Mbilinyi alieleza umuhimu wa waajiri kuwalipia michango wafanyakazi
wake kama sheria inavyotaka, ili kuwawekea akiba pindi wapatapo na majanga
wakiwa kazini.
Akizungumza
wakati akitoa mada Afisa Matekelezo Bi. Amina Likungwala amesema, Mfuko umeamua
kuandaa semina hiyo ili kutoa elimu zaidi kwa waajiri kwa kutambua kuwa waajiri ndio wadau wakuu wa
Mfuko huo na semina hiyo itawasaidia kujua kazi za Mfuko lakini pia wajibu wa
waajiri kwa wafanyakazi katika kutoa michango ya kila mwezi.
Nae, Afisa Madai
wa Mfuko huo, Bi Grace Tarimo alisema Mfuko huo upo kisheria ili kutoa fidia
kwa wafanyakazi watakaoumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi.
Mfuko wa
Fidia kwa wafanyakazi ni Taasisi ya Serikali chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na
umeundwa kwa mujibu wa kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa wafanyakazi Sura
ya 263 iliyorejewa Desemba, Mwaka 2015.
No comments:
Post a Comment