HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, May 12, 2017

Waziri Mwakyembe aipongeza Klabu ya Afrika Lyon kwa kuwa Wazalendo.

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akifafanua jambo wakati wa kikao na uongozi wa Klabu ya michezo ya Afrika Lyon katika  ukumbi wa Idara ya Habari maelezo leo Jijini Dar es Salaam, kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Patrick Kipangula na kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Klabu ya afrika Lyon Bw.Rajuu Kagenzi.
 Mtendaji Mkuu wa Klabu ya afrika Lyon Bw.Rajuu Kagenzi (kushoto) akiongea wakati wa kikao na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) na kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Patrick Kipangula  .

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akipokea jezi kwa niaba ya Rais Dkt.John Pombe Magufuli kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya afrika Lyon Bw.Rajuu Kagenzi (kushoto) mara baada ya kikao na uongozi huo leo Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akionyeshwa michora ya ramani za viwanja vya michezo vinavyotarajiwa kujengwa kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya afrika Lyon Bw.Rajuu Kagenzi (kushoto) leo Jijini dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa uongozi wa Klabu ya michezo ya Afrika Lyon katika  ukumbi wa Idara ya Habari maelezo leo Jijini Dar es Salaam. (Picha na Lorietha Laurence-WHUSM)




Na Lorietha Laurence
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe  ameupongeza uongozi wa Klabu ya michezo ya Afrika Lyon kwa kutumia  mchezo wa mpira wa miguu kuelimisha jamii kupambana na ujangili wa tembo.
Waziri Mwakyembe ametoa pongezi hizo leo Jijini Dar es Salaam wakati alipokutana na uongozi wa klabu hiyo katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO.
Katika kikao hicho uongozi wa timu hiyo ulimueleza Waziri kuwa timu yao imeamua kushiriki vita dhidi ya vitendo vya mauaji ya tembo kwa kuandika ujumbe maalum katika jezi za timu hiyo kuelimisha jamii dhidi ya vitendo hivyo.  
“ni jambo zuri kuhakikisha jamii inapata burudani ya mpira wakati huo huo inaelimika kupitia ujumbe unatolewa na wachezaji katika jezi zao”Dkt Mwakyembe alisema.
Kwa hivyo, aliushukuru uongozi wa timu hiyo kwa juhudi zao hizo na kukieleza kitendo hicho kuwa ni “cha mfano na kujivunia”.
Aliongeza kuwa Serikali inajivunia na kuthamini mchango wa wananchi wazalendo wanaojitolea kujenga taifa na kulinda rasilimali zake kama timu ilivyofanya timu hiyo.
Aidha Waziri  Dkt. Mwakyembe aliongeza kuwa ni jambo jema linalofanywa na klabu hiyo katika kuhakikisha  inakuza  na kuendeleza vipaji kwa vijana mbalimbali nchini jambo ambalo linasaidia kuinua sekta ya michezo.
Pia aliwapongeza kwa kupata fursa ya kutembelea nchi ya China kwa ajili ya kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu michezo na kuwataka kuitumia fursa hiyo ipasavyo kwa kujifunza kwa bidii ili watakaporejea waweze kufundisha vijana wengine wa kitanzania.
Naye Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Afrika Lyon Bw. Rajuu Kangezi ameeleza kuwa mkakati wa klabu hiyo ni kuhakikisha kuwa inajenga viwanja vya michezo vya kisasa kwa matumizi ya jamii ili kuendeleza michezo nchini  hivyo ameomba ushirikiano na serikali katika kufanikisha mikakati hiyo.
“Tuna mipango mingi ya kuhakikisha tunakuwa na viwanja vizuri vya michezo na hili haliwezi kufanikiwa bila kuishirikisha serikali na viongozi wake hivyo tunaomba ushirikiano wa serikali katika kuhakikisha tunafanikisha jambo hili”
Katika kikao hicho uongozi wa klabu hiyo ulimkabidhi Waziri Mwakyembe jezi namba tano “5” ya klabu hiyo kwa ajili ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad