HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, May 23, 2017

WATU 19 WAUWAWA KATIKA SHAMBULIZI LA MANCHESTER ARENA

Watu 19 wameuwawa na wengine zaidi ya 50 wamejeruhiwa katika tukio linashukiwa kuwa ni shambulizi la kigaidi katika ukumbi wa Manchester Arena.

Mlipuko huo umetokea usiku wa jana wakati wa tamasha la muziki la mwanamuziki wa pop kutoka Marekani Ariana Grande.

Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May ametoa pole kwa wafiwa na waliojeruhiwa na tukio hilo ambalo polisi wanalichukulia kama shambulizi la kigaidi.
                         Mwanaume aliyejeruhiwa katika shambulizi la Manchester Arena
          Watu waliokuwa kwenye tamasha wakijifunika na mifuko ya foili kujizuia na baridi

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad