Sheikh Shariff Majini kutoka jijini Dar es salaam ambaye kwa sasa yupo ziarani katika baadhi ya mikoa Tanzania Bara, Jumapili tarehe 28-05-2017 atafanya kongamano kubwa kwa ajili ya akina Mama wa Jijini Arusha katika ukumbi wa CCM Mkoa kuanzia saa mbili asubuhi.
Matayarisho yote yamekwisha malizika na Sheikh ameshawasili Jijini Arusha tayari kabisa kwa ajili ya kuendesha kongamano hilo.
Pamoja na kongamano hilo Sheikh atafanya visomo kwa ajili ya kuwaombea watoto wanafunzi wa Shule ya Lucky Viscent ya Arusha waliofariki katika ajali ya gari. Pamoja na watoto watatu walionusurika wanaopata matibabu Marekani ili wapate nafuu haraka waweze kurejea kwenye masomo yao.
No comments:
Post a Comment