Na Humphrey
Shao, Globu ya Jamii
Kamati ya
Miss Tanzania kwa kushirikiana na kampuni ya Grace Product na Gift Jewelers
wamekabidhi gari kwa Mrembo wa Shindano hilo Diana Edward Lukumai ambaye alishinda taji la Miss Tanzania
2016/2017.
Akizungumza wakati
wa kukabidhiwa zawadi hiyo Miss Diana amesema kuwa anaishukuru sana kamati hiyo kwa kumsaidia kupata zawadi hiyo ambayo ameisubiri kwa hamu na kwa muda mrefu .
“Wasichana
wanatakiwa kuwa wavumilivu na kujiandaa kisaikolojia kwani kushinda taji la
urembo la Miss Tanzania sio kitu kidogo, watu wengi watakufuatilia, hivyo
lazima ujitambue kuwa ukiwa Miss Tanzania ni mtu ambaye anatakiwa kuwa
msiri, hivyo wasichana wajiandae sana kisaikolojia katika hili.” Amesema
Miss Diana.
Amesema kuwa
gari hiyo itaweza kumsaidia katika matumizi yake binafsi hasa katika kipindi
hiki ambacho anaendelea na kampeni yake ya Dondosha wembe ambayo ina lengo la
kumkomboa mtoto wa kike juu ya mila
potofu za kuozeshwa mapema na ukeketaji.
Kwa upande
wake mkuu wa itifaki wa kamati ya Miss Tanzania, Albart Makoye amesema mara
baada ya kukabidhi kwa zawadi hiyo kunafungua pazia la shindano jipya la mwaka
2017/2018 .
Amesema kuwa
warembo wanatakiwa kujiweka sawa hili waweze kunyakuwa taji hilo ambalo
mashindano yake yataanza kuanzia ngazi ya votongoji mpaka taifa.
Ofisa wa Basata akikabidhi funguo kwa Miss Tanzania 2016/2017 Diana Lukumai kama ishara ya kumkabidhi mrembo huyo gari yake aina ya Suzuki Swift pembeni yake Mkurugenzi wa Grace Products Ltd Elizabeth Kilili.
Miss Tanzania 2016/2017 Diana Lukumai akiingia ndani ya gari yake mara baada ya kukabidhiwa
Miss Tanzania 2016/2017 Diana Lukumai akifurahi mara baada ya kuingia ndani ya gari yake
Mkuu wa Itifaki wa Kamati ya Miss Tanzania , Arbart Makoye akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi gari
Mkurugenzi wa Grace Products Ltd Elizabeth Kilili na Mumewe wakikabidhi kadi ya gari kwa Miss Tanzania 2016/217 Diana Lukumai
Mkurugenzi wa Grace Products Ltd Elizabeth Kilili. akizungumza na Miss Tanzania 2016/2017 Diana Lukumai katika duka la ke lililopo City Mall jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment