HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, May 19, 2017

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MKUTANO WA MAKATIBU MAHUSUSI MJINI DODOMA


  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia kwenye mkutano wa mwaka wa 5  wa Chama cha Makatibu Mahususi Tanzania (TAPSEA) uliofanyika kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Jakaya Kikwete ,mjini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)


 Sehemu ya wajumbe waliohudhuria Mkutano Mkuu wa Chama Cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA) ambao mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan(kulia) akizungumza jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki leo kwenye ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA).

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kufanya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA).

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amewaagiza Makatibu Mahsusi nchini kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na waache tabia ya kutoa siri za ofisi zao kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo wakati anafungua mkutano wa Tano wa Chama cha Makatibu Mahsusi Tanzania katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Mji Dodoma.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema uadilifu na uaminifu ni njia pekee ya kuaminiwa na viongozi wao hivyo ni muhimu kwa makatibu mahsusi nchini kufanya kazi kwa bidii na ubunifu mkubwa katika maeneo yao ya kazi.
Makamu wa Rais pia amewahimiza makatibu mahsusi kufanya tathmini ya utendaji wao wa kazi na wawe tayari katika kujifunza mbinu mpya za utendaji zinazoendana na mabadiliko ya teknolojia.
“Sote tunafahamu kuwa dunia imekuwa ni kijiji kutokana na utandawazi unaoletwa na mifumo ya teknolojia hivyo kutokana na mabadiliko haya hamna budi nanyi kubadilika na kwenda na wakati ili msiangaliwe kwa mtazamo hasi wa kuwa wapiga cha tu”
Kuhusu uanzishwaji wa Shahada ya Uhazili, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amewahakikishia makatibu mahsusi kuwa Serikali imekubali kuanzisha shahada hiyo ambapo masomo yake yataanza mwezi wa Tisa mwaka huu kwenye Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania katika mikoa ya Dar es Salaam na Tabora.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amewahimiza makatibu mahsusi kuchangamkia fursa hiyo kwa ajili ya kujiendeleza kielimu kwa kuzingatia kuwa elimu haina mwisho.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Angellah Kairuki amesema Serikali inafanyia kazi baadhi ya kero zinazowakabili makatibu mahsusi ikiwemo kuboresha maslahi ya kada ya uhazili nchini.
Amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha kada hiyo pamoja na watumishi wengine wanapata maslahi bora ambayo yatasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuongeza ufanisi kazi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad