HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, May 1, 2017

DKT. SHEIN AONGOZA SHEREHE ZA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI (MEI MOSI) MAHONDA, ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) pamoja na Viongozi mbali mbali wakishikana mikono kuonesha ishara ya Mshikamano wakati wimbo maalum wa siku ya Wafanyakazi Duniani ukiimbwa katika kilele cha Maadhimisho ya Sherehe zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akipokea Taarifa ya Mwenyekiti wa Chama cha Waaajiri Zanzibar ZANEMA Bw.Salah A.Salah wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya Kilele cha Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimkabidhi zawadi Nd,Asia Ismail Mohammed kutoka ZUPHE katika Ofisi ya Rais Ikulu,Cheti na Fedha Tasilim Shilingi za Kitanzania Laki sita (600,000.00) katika sherehe za kilele cha siku ya Wafanyakazi Duniani (MEI DAY) zilizofanyika leo viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B "Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akiwapungia Mkono Wafanyakazi mbali mbali waliopita mbele yake kwa Maandamano wakati wa Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja akiwa na Viongozi mbali mbali.
Wafanyakazi na Wananchi kutoka shehia mbali mbali za Unguja walijumuika kwa pamoja katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja,wakipita kwa maandamano mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) akiwa mgeni rasmi katika sherehe hizo.
Wafanyakazi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakibeba Bango lenye Nembo la Idara yao wakati wa maandamano katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja,ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani).
Wafanyakazi wa Benki ya Tanzania BOT wakibeba Bango lenye Nembo la Idara yao wakati wa maandamano katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja,ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani).
​Wafanyakazi wa ​Idara ya Uhamiaji Zanzibar wakimpungia Mkono ​Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani),​alipokuwa akipokea ​​maandamano katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja.Picha na Ikulu, Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad