HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, May 12, 2017

BALOZI DK.MAHIGA AKABIDHIWA MAGARI NA SERIKALI YA KUWAIT

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa  Balozi Dk. Augustine Mahiga amepewa msaada wa magari kutoka serikali ya Kuwait ilikuweza kusaidia katika shughuli mbalimbali za kiutendaji.
Balozi Mahiga amesema hayo wakati akipokea msaada wa magari kwa ajili ya wizara yake amesema wizara yake sio yenye tatizo ya usafiri bali ni suala wizara mbalimbali na taasisi zingine za serikali .
Amesema serikali ya Kuwait inatoa msaada katika serikali ya Tanzania zaidi ya dola za kimarekani milioni 200 kwa kila mwaka.
Balozi Mahiga amesema ubalozi wa Kuwait nchini amekubali kusaidia magari kwa sekta zingeni kwa kutaka kuorodhesha mahitaji ya usafiri ili kuweza kusaidia serikali ya Tanzania Kiutendaji.
 Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga  akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kukabidhiwa magari kutoka ubalozi wa Kuwait nchini leo Jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem akizungumza na waandishi wa habari  leo jijini Dar es Salaam katika hafla ya kukabidhii magari yenye thamani ya dola za Kimarekani 100,000 leo jijini Dar es Salaam.picha zote na Emmauel Massaka,Glob ya Jamii.
  Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem akikabidhi funguo za Magari kwa Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga katika hafla iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
  Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiteta jambo na Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem
 Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa wizara hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad