Mzee
Francis Maige Ngosha (kwenye kitanda) akitolewa katika Hospitali ya
Rufaa Amana tayari kwa kupelekwa Hosptali ya Taifa Muhimbili kwa ajili
ya matibabu zaidi.
Na Anthony John Globu ya Jamii.
Na Anthony John Globu ya Jamii.
Serikali imeahidi kumpatia matibabu Mzee Francis Ngosha aliyebuni Nembo ya taifa. Hatua hiyo imekuja baada ya kituo cha Runinga cha ITV Dar es salaam kumuonesha mzee huyo akiwa katika hali mbaya katika eneo Buguruni ambapo alikutwa akiishi kwenye chumba kimoja alichopewa na msamaria mwema.
Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo hii katika hospitali ya Rufaa ya Amana DKT, Hamisi Kigwangalla amesema mchango wamzee huyu ni mkubwa ambao utakumbuka na vizazi vyote nchini kwa suala hilo alilolifanya.
Aidha Kigwangalla amesema kuwa serikali ilipata tarifa juu ya madhira anayoyapata hivyo serikali ilimuagiza kuchukua hatua za haraka za kumsaidia mzee huyu.
‘’Katika hatua hii tunashughulika na suala matibabu na baada ya matibabu kukamilika tutamtafutia makazi ya kuishi kama atakubali atapelekwa katika nyumba ya wazee wasiojiweza iliyopo Nunge au tumtafutie nyumba kwaajili ya kuishi’’amesema Kigwangalla.
Mzee Francis Maige Ngosha (kwenye kitanda) akiwa kwenye gari la wagonjwa tayari kwa kupelekwa Hosptali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu zaidi. (Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii).
Naibu Waziri,Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.Hamisi Kigwangalla akimjulia hali Mzee Francis Maige Ngosha aliyelazwa kwenye wodi ya Wanaume Hospitali ya Rufaa Amana leo jijini Dar es Salaam.
Mzee Francis Maige Ngosha (kwenye kitanda) akiwa kwenye gari la wagonjwa tayari kwa kupelekwa Hosptali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu zaidi. (Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii).
Naibu Waziri,Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.Hamisi Kigwangalla akimjulia hali Mzee Francis Maige Ngosha aliyelazwa kwenye wodi ya Wanaume Hospitali ya Rufaa Amana leo jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Dk. Hamisi Kigwagalla akiongea na waandishi wa habari kuhusu hatua waliyochukua ya kumuhamishia Mzee Maige kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Dharura Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt. Juma Mfinanga akizungumza na Mzee Francis Maige mara baada ya kupakiwa kwenye gari ya kubeba wagonjwa tayari kwa kupelekwa Muhimbili leo jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment