HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, April 14, 2017

WATANZANIA WAISHIO ALGERIA WAUPOKEA MSAFARA WA YANGA KWA SHANGWE


 Kikosi cha wawakilishi watanzania katika michuano ya kimataifa ya kombe la Shirikisho barani Afrika Yanga wamewasili salama nchini Algerai kwa ajili ya mchezo wao marudiano dhidi ya MC Alger utakaochezwa kesho majira ya saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

Katika msafara huo uliiongozwa na Katibu Mkuu wa Yanga Charles Boniface Mkwasa umefika salama na ukipokelewa na watanzania wanaoishi nchi Algeria na kufurahishwa na mapokezi hayo na kuahidi ushindi kwa watanzania.

Msafara wa wachezaji hao uliingia kwa mafungu mawili ambapo kundi la kwanza liliwasili likiongozwa na benchi la ufundi la timu hiyo likiwa na kocha Mkuu George Lwandamina huku kundi la pili likiwasili  na Katibu Mkuu.

Mtanzania Hamis Mwampese anayeishi nchini Algeria amesema kuwa timu ya Algers wameingia uoga hasa baada ya kuona Yanga wamechelewa kuingia nchini humo na zaidi kwa kufanya hivyo wameepusha sana kufanyiwa hujuma na wenyeji wa nchi hiyo.

Yanga wamefikia katika Hotel ya nyota tano inayojulikana kwa jina la Sultan ambapo si mbali sana na Uwanja ulipo utakaochezewa kesho katika mechi hiyo ya marudiano ambapo Yanga wanatakiwa kupata ushindi wa aina yoyote au sare.

Mtanzania Hamis Mwampese akisalimiana na Katibu Mkuu wa Yanga Charles Mkwasa baada ya kuwasili Jijini Algeria  kwa ajili ya mechi ya marudiano ya hatua ya mtaoano wa Kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Mc Alger ambapo katika mechi ya awali Yanga walitoka na ushindi wa goli 1-0..
 
Mtanzania Hamis Mwampese  akiwa katika picha mbalimbali na wachezaji wa timu hiyo baada ya kuwasili nchini Algeria kwa ajili ya mechi ya marudiano ya hatua ya mtaoano wa Kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Mc Alger ambapo katika mechi ya awali Yanga walitoka na ushindi wa goli 1-0.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad