HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, April 6, 2017

TANZANIA YAPANDA HADI NAFASI YA 135, BRAZIL YASHIKA NAMBA MOJA DUNIANI



SHIRIKISHO la Soka Duniani (FIFA) limetoa viwango bora vya soka duniani kwa nchi zote huku Brazil wakiwashika namba moja wakifuatiwa na Argentina na Ujerumani iliyoshika nafasi ya tatu.


Katika viwango hivyo bora vya soka, timu ya Misri iliweza kuingia katika 20 bora kwa kushika nafasi ya 19 na Senegal kushika nafasi ya 30 duniani.

Kulingana na ratiba ya mechi za Kirafiki za kalenda ya FIFA, Tanzania imefanikiwa kupanda kwa nafasi 22 kutoka 157 mpaka nafasi ya 135 .


Kwa upande wa nchi za Afrika Mashariki, Uganda imeendelea kuongoza lakini wakipanda  kwa nafasi 2 kutoka 74 mpaka 72 akifuatiwa na Kenya iliyo nafasi ya 78, Rwanda nafasi ya 117 na Burundi 141.

Viwango vingine vitatolewa Mei mwaka huu.


MATAIFA YA AFRIKA 10 YENYE VIWANGO BORA VYA FIFA AFRIKA MWEZI HUU . 


1. Misri ( 19 )

2. Senegal ( 30 )

3. Cameroon ( 33 )

4. Burkinafaso ( 35 )

5. Nigeria ( 40 )

6. Congo DR ( 41 )

7. Tunisia ( 42 )

8. Ghana (45 )

9. Ivory Coast ( 48 )

10. Morocco ( 53 )

MATAIFA 10  YENYE VIWANGO BORA VYA FIFA MWEZI HUU

1Brazili 

2.Argentina 

3.Ujerumani

4.Chile

5.Colombia

6.Ufaransa

7.Ubelgiji

8.Ureno

9.Uswisi

10.Hispania

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad