HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, April 21, 2017

DKT. GHALIB BILAL KUWA MGENI RASMI UZINDUZI WA KAMPENI YA KILL CHALLENGE 2017

MAKAMU wa Rais mstaafu wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt Mohamed  Ghalib Bilal anatarajia kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa kampeni ya Kill Challenge kwa mwaka 2017, kampeni hiyo yenye lengo la kukusanya fedha kwa ajili kusaidia mapambano dhidi ya maambukizi ya vurusi vya Ukimwi.

Kampeni hiyo ambayo imeandaliwa na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) kwa kushirikiana na Tume ya kupambana na virusi vya Ukimwi  nchini (TACAIDS).

Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam leo, Makamu wa Rais wa mradi endelevu wa Mgodi (GGM), Simo Shayo amesema uzinduzii huo utafanyika kwenye Hotel ya kimataifa  Kilimanjaro  Hoteli .

‘’Nawakalibisha watu wote kujitokeza katika kuchangia fedha hizi ili zisaidie katika kupambana na maambuzi haya, kwani jukumu la kupambana na ugonjwa huu sio wa serikali peke yake bali hata jamii nzima inahaja ya kujitokeza na kupambana na ugonjwa huu’’Amesema Shayo.

Shayo amebainisha kuwa  katika kampeni hiyo wameshirikiana na wasanii akiwemo Mrisho  Mpoto kwa lengo la kuiamsha jamii ili ijitokeze katika kupambana na vita hiyo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa (TACAIDS)Dkt Leonard Maboko amewasihi Makampuni mengine yaige mfano  wa (GGM) Katika kuhakisha watahakikisha ugonjwa wa Ukimwi unatokomezwa nchini.
Makamu wa Rais wa miradi endelevu wa Mgodi (GGM), Simo Shayo akizungumza na waaandishi wa habari (hawapo pichani) juu uzinduzi wa kampeni ya Kill Challenge kwa mwaka 2017, leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa (TACAIDS), Dkt. Leonard Maboko naye akizungumzia Kampeni hiyo katika mkutano ulio fanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mwanamziki maarufu nchini, Mrisho Mpoto ambaye ni Balozi wa Kampeni ya Killchalange 2017 amapo amewasihi wasanii wenzake kujitokeza na kuungana naye katika vita ya kupambana dhidi ya maambuki ya virusi vya Ukimwi.leo jijini Dar es Salaam.
Watendaji wa (TACAIDS) na waandishi wa habari wakimsikiliza Makamu wa Rais wa miradi endelevu wa Mgodi (GGM) ,Simo Shayo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad