HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, April 18, 2017

BALOZI WA MSUMBIJI AKUTANA NA TCCIA KUIMARISHA MAHUSIANO YA BIASHARA KATI YA TANZANIA NA MSUMBIJI

Balozi wa Msumbiji nchini Bi Monica Patricio Clemente akizungumza na viongozi wa TCCIA walioongozana na Makamu wa Rais-Viwanda Bw. Octavian Mshiu wa kwanza kulia, Mkurugenzi Mtendaji Bw. Gotfrid Muganda pamoja na viongozi wa TCCIA Mtwara Bw. Swallah S. Swallah-Mwenyekiti na Muhidin Swalehe. 
Mkutano huo ulihudhuriwa na Makamu wa Rais wa TCCIA mwenye dhamana ya Viwanda Bw. Octavian Mshiu akiambatana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TCCIA Bw. Gotfrid Muganda pamoja na viongozi wa TCCIA Mkoa wa Mtwara Bw. Swallah S. Swallah ambaye ni Mwenyekiti na Bw. Muhidin Swalehe- Afisa Mtendaji.Akizungumza katika mkutano huo, Makamu wa Rais wa TCCIA- Viwanda Bw. Octavian Mshiu amesema mapendekezo ambayo TCCIA imewasilisha kwa Balozi wa Msumbiji nchini yanalenga kutoa ushirikiano wa karibu kwa wafanyabiashara wa pande zote mbili ambao utawezesha uanzishwaji wa vituo katika mkoa wa Mtwara ili kurahisisha upatikanaji wa huduma na misaada ya haraka kwa wafanyabiashara wa pande zote mbili.
Makamu wa Rais wa TCCIA-Viwanda Bw. Octavian Mshiu akimkabidhi Balozi Monica Clemente nyaraka maalum baada ya mkutano na Balozi huyo ofisini kwake mapema wiki iliyopita.
Balozi Bi. Monica Patricio Clemente amesema amefurahishwa na ugeni alioupata wa uongozi wa TCCIA na kwamba mapendekezo chanya yaliyoletwa na TCCIA yana nafasi sahihi na muhimu katika kuboresha ushirikiano wa wafanyabiashara wa Mtwara na Mikoa jirani ya Msumbiji kwani mahusiano ya aina hiyo yana nafasi kubwa ya kunufaisha jamii ya wafanyabiashara, kuongeza pato la nchi zote mbili na pia kukuza uchumi wa maeneo husika.
Balozi Monica ameahidi kuyafanyia kazi majadiliano na mapendekezo ya TCCIA kwa haraka ili kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi wa mikoa inayofanya biashara pamoja ambayo matokeo yake yataleta tija kwa maslahi ya Tanzania na Msumbiji kwa ujumla
Viongozi wa TCCIA wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa ubalozi wa Msumbiji nchini baada ya mkutano wa Balozi na uongozi wa TCCIA jijini.
Katika mkutano huo wajumbe kutoka ubalozini humo wamesema moja ya changamoto kubwa inayowakumba wafanyabiashara wengi ni lugha ambapo wamependekeza pia kuwepo kwa vituo maalum ambavyo vitakuwa vikitoa elimu ya lugha kwa wafanyabiashara hao ili kuondoa changamoto hiyo.Mwenyekiti wa TCCIA Mtwara Bw. Swallah S. Swallah ameshukuru ubalozi wa Msumbiji kwa ukarimu na kuahidi kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya wafanyabiashara wa Cape Delgado nchini Msumbiji na Mtwara nchini Tanzania. Pia alieleza juhudi za Chemba ya Mtwara katika kukabiliana na changamoto ya lugha na kwamba mjini Mtwara tayari kuna kituo kikubwa cha lugha kinachofundisha watanzania lugha mbalimbali ikiwemo Kireno ambacho sasa kinatiliwa mkazo zaidi.
Viongozi wa TCCIA wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa ubalozi wa Msumbiji nchini baada ya mkutano wa Balozi na uongozi wa TCCIA jijini.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad