Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa
Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi,
Arch, Dk. Ambwene Mwakyusa akizungumza na waandishi wa habari leo jijini
Dar es Salaam kuhusiana maandalizi ya semina endelevu ya Bodi ya 27,
itakayofanyika tarehe 23-24, machi 2017 katika ukumbi wa Rock City Mall Mwanza.
Ambapo
amesema lengo la semina hiyo ni kuwaelimisha Wabunifu Majengo, Wakadiriaji
Majenzi na Wataalam wanaoshabihiana nao pamoja na wadau kutoka sekta ya ujenzi
ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya sayansi na teknologia na kubadilishana
changamoto za utandawazi.
Mgeni
rasmi katika semina hiyo anatarajiwa kuwa Waziri wa
Ujenzi, Uchukuzi
na Mawasiliano
Profesa Makame Mbarawa.
KAULI
MBIO YA SEMINA HIYO.
"Mchango
Unaotokana na Ushirikiano wa Serikali na Sekta Binafsi, Pamoja na Taasisi za
Fedha katika kuendeleza Sekta ya Ujenzi ('The
Contribution of Public Private Partneship anda Financial Institutions in the
Development of the Construction Industry)
No comments:
Post a Comment