Wakala
wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) umeandaa maboresho ya ujumla ya
mfumo mzima wa usajili chini ya Mkakati wa Kitaifa wa Kuboresha Usajili
wa Matukio Muhimu ya Binadamu na Takwimu (National Strategy on Civil
Registration and Vital Statistics - kwa kifupi National CRVS Strategy),
ili kuisaidia Serikali kupata takwimu sahihi za wananchi zinazoisaidia
kupanga mipango ya maendeleo na huduma za jamii. Kwa mujibu wa Takwimu
za Sensa ya mwaka 2012 ni asilimia 13.4 ya Wananchi ndiyo waliyosajiliwa
na kupata vyeti vya kuzaliwa.
Hayo
yamesemwa na Kaimu Afisa Mtendaji wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na
Udhamini (RITA), Emmy Hudson, wakati wa Mkutano wake na baadhi ya
wahariri na waandishi wa habari, uliofanyika kwenye makao makuu ya RITA,
jijini Dar es salaam.
Alisema
Mkakati huo wa CRVS una mipango mbalimbali ya utekelezaki ikiwa ya muda
mfupi na mrefu kwa makundi yatokanayo na umri ili kufikia ufanisi
unaotarajiwa. Makundi hayo ni la Watoto wa Umri chini ya miaka mitano,
kundi la watu miaka 5 - 17 na kundi la wananchi wa miaka 18 na
kuendelea, ambapo Utekelezaji wa Usajili kwa kundi la kwanza umeshaanza
kupitia Mpango wa Usajili wa Watoto wa Umri Chini ya Miaka Mitano ambapo
kwa sasa unatekelezwa katika Mikoa mitano ya Tanzania Bara ambayo ni
Mwanza, Mbeya, Songwe,Iringa na Njombe.
Kaimu
Afisa Mtendaji wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Emmy
Hudson akizungumza na baadhi ya wahariri na waandishi wa habari
waliofika katika Makao makuu yake Jijini Dar es salalaam leo, wakati
akizungumzia Mkakati wa Kitaifa wa Kuboresha Usajili wa Matukio Muhimu ya Binadamu hapa nchini.
Kaimu Afisa Mtendaji wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Emmy Hudson akiendelea kuzungumza na wanahabari hao.
Mkurugenzi wa TEHAMA wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Cuthbert Simalenga akifafanua jambo katika Mkutano huo.
No comments:
Post a Comment