HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, March 1, 2017

NYUMBA ZA MAGOMENI COTTERS KUKAMILIKA MWEZI SEPTEMBA

 Eng. Athu Chulla akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani (wa pili kulia), mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba zinazojengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), katika eneo la Magomeni jijini Dar es Salaam. Pembeni kwa Naibu Waziri ni Mratibu wa Ujenzi wa nyumba hizo, Arch. Christina Shayo.
 Mratibu wa Ujenzi wa nyumba  zinazojengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Arch. Christina Shayo (wa kwanza kushoto), akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani,  mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba katika eneo la Magomeni jijini Dar es Salaam.
 Muonekano wa moja ya nyumba za wananchi zinazojengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) katika eneo la Magomeni ikiwa katika hatua ya msingi, Nyumba hizo zinatarajiwa kuhudumia kaya 656 zitakapokamilia Septemba mwaka huu.
Mafundi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), wakiendelea na ujenzi wa nyumba za wananchi katika eneo la Magomeni. Nyumba hizo zinatarajiwa kuhudumia kaya 656 zitakapokamilia Septemba mwaka huu.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad