HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, March 2, 2017

NAIBU KAMISHNA MKUU WA SHIRIKA LA FORODHA LA KOREA ATEMBELEA TRA

 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Alphayo Kidata (kulia) akimkaribisha Naibu Kamishna Mkuu wa Shirika la Huduma za Forodha la Korea (Korea Customs Service-KCS) Dk. Jong-Yeul Kim alipotembelea TRA tarehe 1 Machi 2017 ili kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya taasisi hizo. Baadhi ya mambo waliyojadili ni pamoja na  utekelezaji wa mradi wa Dirisha Moja la Huduma (Electronic Single Window Systems) kufuatia makubaliano ya ushirikiano  yaliyofanyika baina ya taasisi hizo mbili.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Alphayo Kidata (kulia) akimuelezea jambo Naibu Kamishna Mkuu wa Shirika la Huduma za Forodha la Korea (Korea Customs Service - KCS) Dk. Jong-Yeul Kim alipotembelea TRA tarehe 1 Machi 2017 ili kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya Taasisi hizo mbili.
  Naibu Kamishna Mkuu wa Shirika la Huduma za Forodha la Korea (Korea Customs Service-KCS) Dk. Jong-Yeul Kim  (aliyeshika picha kushoto) akifurahia moja ya zawadi aliyokabidhiwa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Alphayo Kidata (kulia) mara baada ya kumaliza mkutano wa pamoja  uliofanyika katika ofisi ya TRA Makao Makuu wakati wa ziara ya Dk. Kim nchini Tanzania.
Timu ya  Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) (kulia) ikiongozwa na Kamishna Mkuu Bw. Alphayo Kidata   pamoja na Timu ya Shirika la Huduma za Forodha la Korea (Korea Customs Service-KCS)  ikiongozwa na  Naibu Kamishna Mkuu Dk. Jong-Yeul Kim walipokutana katika ofisi ya TRA Makao Makuu ili kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya taasisi hizo mbili.
 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Alphayo Kidata (wa nne kulia)  pamoja na Naibu Kamishna Mkuu wa Shirika la Huduma za Forodha la Korea (Korea Customs Service-KCS) Dk. Jong-Yeul Kim (wa tano kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kikao cha pamoja kilichowakilisha taasisi hizo mbili. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad