HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, March 29, 2017

MKUU WA WILAYA YA CHEMBA AZINDUA ZOEZI LA UTHAMINI

 Mkuu wa Wilaya ya Chemba Ndugu Simon Ezekiel Odunga akizungumza na wananchi wa kata ya Farkwa wakati wa uzinduzi wa zoezi la uthamini mali ili kupisha ujenzi wa bwawa la Farkwa.
Mkuu wa Wilaya ya Chemba mkoani Dodoma akiongozana na baadhi wa Viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, Wataalamu wa Halmashauri, Wataalamu kutoka Wizara ya Maji, Uvuvi na umwaguliaji,  Wataalamu wa Bonde la Kati na Wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wamezindua zoezi la uthamini wa mali za wananchi wa vijiji viwili vya Mombose na Bubutole watakaohama kupisha mradi mkubwa wa Ujenzi wa bwawa la Farkwa mkoani hapa.

Mradi wa bwawa la Farkwa ni mradi mkubwa ambao huenda ukawa ni mkubwa katika Ujenzi wa mabwawa makubwa kuliko yote barani Afrika. Mradi huu uliasisiwa na baba wa Taifa tangu mwaka 1970 utazinufaisha Wilaya za Bahi, Chemba, Chamwino na Dodoma Manispaa na utegemea kutumia pesa za Tanzania zaidi ya Tilioni 2.

Kufuatia umuhimu wa mradi huu na uwijio wa makao makuu ya nchi mkoani Dodoma, serikali imezamilia ifikapo mei mwaka huu zoezi la Uthamini wa mali za wananchi wanaohama kupisha mradi huu mkubwa katika Vijijini vya Mombose na Bubutole vilivyopo Wilayani Chemba pamoja na vijiji vinavyopitiwa na njia Kuu ya bomba linalopeleka Maji eneo la Kilimani mjini Dodoma liwe limekamilika tayari kwa kuwalipa wananchi ili Ujenzi wa bwawa uanze.

Ujenzi wa mradi huu unategemea kuchukua miaka mitatu 2017-2021 mpaka kukamilika kwake. Hivyo wananchi wametakiwa kutoa ushirikiano kwa Wataalamu wa uthamini kwa kuwa wameusubiri mradi huu kwa zaidi ya miaka 47 na leo serikali imepata fedha ya kuutekeleza.

Mhe Mkuu wa Wilaya ya Chemba Ndugu Simon Odunga wamewataka wananchi hao kujiepusha na watu wasiopenda maendeleo yao na nchi yetu kwa ujumla wa anaopita pita huko na kujifanya watetezi wa haki za wananchi. Swali hao watetezi walikuwa wapi tangu 1970 waje leo ambapo mradi unaanza kutekelezwa.?

Aidha, amesisitiza wananchi ambao ni wamiliki halali wa maeneo husika ndio wajitokeze kwenye uthamini huo ili kuepusha udanganyifu na migogoro isiyo ya lazima wakati wa malipo yatakopoanza. Kwani kuna baadhi ya wananchi zi waaminifu na atakayefanya hivyo akibaini sheria kali dhidi yake zitachukua mkondo.

Kwa upande wa Wataalamu Mkuu huyo wa Wilaya amewataka kutumia akili, uweledi na taaluma zao katika kuhakikisha kila mwananchi wa maeneo hayo anapata haki yake stahiki kwa mujibu wa sheria za uthamini.

Katika Mkutano huo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, Mhe Rajabu Muheshimwa ameongea kwa kupongeza juhudi za Serikali kwa kuamua kuanza mradi huu na zaidi kusihi wananchi kutoa ushirikiano kwa Wataalamu, hali kadhalika Mhe  Diwani wa Kata ya Farkwa Ndugu, Suleiman Gawa amesisitiza kuhakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu pia Wataalamu wahakikishe wanaorodhesha mali zote za wananchi zinazotambulika kisheria ili kuepusha migongano hapo baadae.

Naye Katibu Tawala wa Wilaya amewataka Viongozi wa Vijiji na vitongoji kusimamia zoezi hili kikamilifu kwani wao ndio wanaowafahamu  wananchi wao pia watoto ambao wanamiliki mali lakini hawatambuliwi kisheria kutokana na umri wao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad