HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, March 1, 2017

KIMENUKA, KAMATI YA UTENDAJI YANGA WAKUTANA KUJADILI MUSTAKABALI WA KLABU HIYO

Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga

Na Mwandishi Weu, Globu ya Jamii

VIONGOZI wa kamati ya Utendaji wa Yanga wakutana leo kujadili masuala mbalimbali ya klabu hiyo kutokana na kuwa katika hali ngumu ya ukata inayoikabili.

Kutoka ndani, kikao huo ulioanza toka asubuhi kimekuwa cha siri sana wakiwa katika majadiliano makali na pia ikionekana kutaka kuinusuru klabu hiyo kutoka kwenye hali hiyo ambapo imepoteza mchezo wa Jumamosi dhidi ya Simba.

Kamati ya Utendaji wa Yanga wameamua kukutana leo ikiwa ni siku mbili baada ya Katibu Mkuu wa Yanga Boniface Mkwasa kuweka wazi hali ya ukata wa klabu hiyo, pia wachezaji kulalamika kuhusiana na kutokulipwa mishahara yao.

Pia, kumekuwa na taarifa kuwa mchezaji wa kimataifa kutokea nchini Zimbambwe kuweka wazi kuwa baadhi ya viongozi walidanganywa kuwa anaweza kucheza katika mechi dhidi ya Simba wakati si kweli.

Mbivu na mbichi za kikao hicho cha kamati ya utendaji kitajulikana baada ya kumalizika na maamuzi hayo ni kwa ajili ya kuiokoa Yanga kuweza kuhakikisha inafa nya vizuri kwenye michezo iliyobaki na kutetea ubingwa wake.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad