Na Mary Gwera - Mahakama
Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu amemtembelea Kaimu Jaji
Mkuu, ambapo amesisitiza juu ya ushirikiano kati ya Mahakama yake na
Mahakama nchini. Rais huyo wa Mahakama ya Afrika, Mhe. Jaji Sylvain ORE` alimtembelea Mhe.
Kaimu Jaji Mkuu mapema Machi 1, katika ofisi zake zilizopo Mahakama ya
Rufani (T) jijini Dar es Salaam, ambapo lengo mojawapo la ujio wake ilikuwa ni
kumpongeza Mhe. Kaimu Mkuu nchini kwa kuteuliwa kwake kushika nafasi hiyo.
Aidha mbali na kutoa pongezi, ujio wake pia umelenga katika kuendeleza
mahusiano yaliyokuwepo wakati wa utawala wa Jaji Mkuu Mstaafu, Mhe.
Mohamed Chande Othman kwani Mahakama mdau mkubwa katika Mahakama hii. Mbali na kumtembelea Kaimu Jaji Mkuu, Rais huyo wa Mahakama ya Afrika ya
Haki za Binadamu alimtembelea pia, Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania,
Mhe. Ferdinand Wambali.
Akitoa maelezo mafupi kwa niaba ya Kaimu Jaji Mkuu kwa mgeni huyo, Mhe.
Wambali alimueleza juu ya muundo wa Mahakama nchini na jinsi inavyofanya
kazi ya utoaji haki nchini. Aliendelea kuongelea juu ya maboresho ya utoaji huduma ya haki kwa wananchi
kwamba nia ya Mahakama ni kuwa na huduma ya Mahakama Kuu kila Mkoa ili
kuwawezesha wananchi wa kila mkoa kupata huduma ya haki.
“Nia ya Mahakama ni kuwa na Mahakama Kuu katika kila mkoa, kwa sasa kuna
zaidi ya mikoa 13 ambayo bado haina Mahakama Kuu, hivyo kwa Mwaka huu wa
fedha Mahakama imepanga kuanza ujenzi wa jumla ya Mahakama Kuu nne, na
tutakuwa tukifanya hivi kwa awamu kadri bajeti itakavyoruhusu,” alieleza Jaji
Wambali.
Mbali na kukutana na Viongozi hao Wakuu wa Mahakama, Rais huyo wa
Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu alipata wasaa wa kujionea muonekano
wa kumbi za Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu ya Tanzania. Rais huyo kutoka nchini Ivory Coast amechukua nafasi iliyoachwa wazi na
aliyekuwa Rais wa Mahakama hiyo, Mhe. Jaji Augustino Ramadhani.
Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Juma (kulia),
akimkaribisha Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu, Mhe.
Jaji Sylvain ORE`, alipowasili ofisini kwake Mahakama ya Rufani (T).
Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu, Mhe. Jaji Sylvain
ORE`, akitia sahihi kitabu cha Wageni alipowasili ofisini kwa Kaimu Jaji
Mkuu wa Tanzania.
Afisa Itifaki, Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu, Bw. Simba
Tamaambele (kushoto) pamoja na Katibu wa Mhe. Kaimu Jaji Mkuu, Mhe.
Elinaza Luvanda wakifuatilia mazungumzo ya Viongozi hao.
Katibu wa Mhe. Kaimu Jaji Mkuu, Mhe. Elinaza Luvanda (kulia)
akimuonesha kitu Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu, Mhe.
Jaji Sylvain ORE` alipotembelea katika Ukumbi namba 1 wa Mahakama ya
Rufani (T).
Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania,Mhe. Ferdinand Wambali
(kushoto) akijadili jambo na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za
Binadamu, Mhe. Jaji Sylvain ORE` (kulia), pindi Rais huyo alipowasili
ofisini kwa Mhe. Jaji Kiongozi, katikati ni Afisa Itifaki, Mahakama ya
Afrika ya Haki za Binadamu, Bw. Simba Tamaambele.
Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania,Mhe. Ferdinand Wambali
(kushoto) akimuonesha kitu Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za
Binadamu, Mhe. Jaji Sylvain ORE` alipokuwa katika Ukumbi namba 1 wa
Mahakama Kuu ya Tanzania.
No comments:
Post a Comment