HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, February 18, 2017

YANGA YASONGA MBELE MASHINDANO YA KLABU BINGWA AFRIKA

Kikosi cha timu ya Yanga kilichocheza na Ng'aya Fc uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jioni ya leo na Mchezo huo kumalizika kwa droo ya kufungana bao 1-1.
Kikosi cha Timu ya Ng'aya Fc ya Comoro kikiwa katika picha ya pamoja katika mchezo wao dhidi ya Yanga, mchezo uliomalizika jioni hii katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 Kipa wa Ng'aya Fc ya Comoro, Said Mmad akidaka mpira mbele ya mabeki wake na washambuliaji wa Yanga.
 Mshambuliaji wa Ng'aya Fc, Said Hachim akiwania mpira wa juu na beki wa Yanga, Kelvin Yondani katika mchezo wa klabu bingwa barani Afrika, uliochezwa jioni ya leo katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, mchezo huo umemalizika kwa sare ya bao 1-1.
 Beki wa Yanga, Vicent Bossou akiokoa mpira mbele ya washambuliaji wa timu ya Ng'aya katika mchezo wa klabu bingwa barani Afrika, uliochezwa jioni ya leo katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, mchezo huo umemalizika kwa sare ya bao 1-1.
 Kiungo wa kati wa Yanga, Thabani Kamusoko akipita katikati ya msitu wa watu mara baada ya kufanikiwa kuchukua mpira kwa kiungo wa timu ya Ng'aya Fc.
 Kipa wa Timu ya Ng'aya akiwa ametanda katika lango lake kwenye mchezo wao dhidi ya Ng'aya ya Comoro
 Mshambuliaji wa Yanga, Obrey Chirwa akijaribu kutka kuchukua mpira mbele mbele ya mchezaji wa Ng'aya Said Toihir
 Beki wa Kulia wa Ng'aya Fc  akiokoa mpira mbele ya mshambuliaji wa Yanga , Deus Kaseke
 Beki wa kushoto wa timu ya Yanga , Mwinyi Haji akishangilia bao lake la kusawazisha dhidi ya Ng'aya Fc ya Comoro.
Wachezaji wa Yanga wakishangilia goli la kusawazisha kwa pamoja
 Simon Msuva akijaribu kutaka kupiga mpira mbele ya glikipa wa Ng'aya Fc ya Comoro
Mabeki wa Ngaya Fc ya Comoro wakiokoa mpira uliopigwa na kiungo wa Yanga , Justin Zulu

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad