HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, February 19, 2017

UUNDWAJI WA MELI MBILI ZA MV NJOMBE NA MV RUVUMA WAKAMILIKA

Meli mbili za Mv. Ruvuma na Mv Njembe zikiwa katika cherezo katika Bandari ya Itungi, Wilayani Kyela Mkoani Mbeya, zikiwa katika hatua za mwisho kabla ya kuanza kufanyiwa majaribio ndani ya Ziwa Nyasa Mwishoni mwa Februari, 2017.
Benny Mwaipaja, WFM, Kyela

UJENZI wa meli mbili za mizigo katika Bandari ya Itungi wilayani Kyela Mkoani Mbeya, MV Njombe na MV Ruvuma, umekamilika kwa zaidi ya asilimia 98 na kwamba meli hizo zinatarajiwa kufanyiwa majaribio Ziwa Nyasa, mwishoni mwa mwezi Februari na kukabidhiwa rasmi Serikalini mwezi Machi, 2017

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Songoro MarineTransport Ltd ya Jijini Mwanza, inayounda meli hizo, Mhandisi Saleh Songoro, amesema hayo wakati ujumbe wa Serikali ulioongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizaya ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Khamis Shaaban, ulipotembelea Bandari hiyo ukiwa katika zaira ya kukagua hali ya biashara mipakani mkoani Mbeya.

Amesema kuwa kukamilika kwa meli hizo mbili za mizigo za kisasa zenye uwezo wa kubeba tani elfu moja (1,000) za mizigo kila moja na kugharimu shilingi bilioni 11, kutaiwezesha Kampuni hiyo kuanza kuunda meli nyingine ya tatu itakayokuwa na uwezo wa kubeba abiria 200 na tani 200 za mizigo.

Pamoja na meli hizo, Mhandisi Songoro amesema kuwa mradi huo pia umewezesha kujengwa kwa cherezo cha kwanza na cha pekee kitakacho iwezesha Mamlaka ya Bandari Tanzania-TPA katika uundaji wa meli na kuzifanyia matengenezo meli nyingine za ndani na nje ya nchi zikiwemo Malawi na Msumbiji.

Kaimu Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Bandari ya Itungi, Bw. Ajuaye Msese, amesema kuwa uamuzi wa Serikali wa kuunda meli hizo ulikuwa kutatua changamoto ya muda mrefu ya ukosefu wa vyombo vya baharini vya kusafirisha abiria na mizingo ndani na nje ya nchi kupitia Ziwa Nyasa.

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, , pamoja na kupongeza kazi kubwa iliyofanywa na mkandarasi mzawa, Songoro Marine Transport Ltd, kuunda meli hizo, wamesema kuwa kukamilika kwa meli hizo kutachochea biashara na mapato ya serikali kupitia shughuli za usafiri na usafirishaji katika Ziwa Nyasa.

Prof. Mkenda amesisitiza kuwa Serikali itaangalia uwezekano namna ya kumtumia Mkandarasi huyo, Bw. Saleh Songoro, kuunda meli nyingi zaidi za ndani na nje ya nchi ili kukamata soko hilo la utengenezaji wa meli kitaifa na kimataifa hatua itakayoliletea Taifa sifa, kukuza uwekezaji na ajira.

Ujenzi wa Meli zote tatu, mbili za mizigo pekee, na moja ya mizigo na abiria, umekadiriwa kugharimu zaidi ya shilingi bilioni 20 na utakuwa umetekeleza ahadi ya Serikali ya muda mrefu ya kuboresha usafiri wa abiria na mizigo kupitia Ziwa Nyasa, ambapo unatarajiwa kukuza biashara kati ya Tanzania, Malawi na Msumbiji, kusisimua uchumi wa wakazi wa wilaya ya Kyela na ukanda wote wa Kusini.

Aidha kukamilika kwa ujenzi wa meli hizo kutapunguza matukio ya ajali za mara kwa mara zinazogharimu maisha ya watu wengi wanaotumia Ziwa Nyasa, linalo tajwa kuwa la pili kwa kuwa na mawimbi makali na la tano kuwa na kina kirefu cha maji duniani.
Bw. Juma Nassoro akipaka rangi meli ya mizigo ya Mv Ruvuma, ikiwa ni hatua za mwisho wa ukamilishaji wa uundaji wa meli hiyo yenye uwezo wakubeba tani 1000 za mizigo itakayokuwa ikifanya safari zake Ziwa Nyasa, wakti Ujumbe wa Serikali kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, ulipofanya ziara katika Bandari ya Itungi, wilayani Kyela mkoani Mbeya.
Kaimu Mkuu wa Bandari ya Itungi, Wilayani Kyela mkoani Mbeya, Bw. Ajuaye Msese akitoa maelezo mafupi kuhusu Bandari ya Itungi, na majukumu yake kwa ujumla kwa wageni waliotembelea Bandari hiyo mkoani Mbeya. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Songoro Marine Transport Ltd, inayounda meli tatu katika Bandari hiyo, Bw. Saleh Songoro, akielezea historia fupi ya kampuni yake iliyoingia mkataba na Mamlaka ya Bandari Tanzania-TPA kuunda meli tatu Ziwa Nyasa, baada ya Ujumbe wa Serikali ukiongozwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Khamis Shaaban, ulipotembelea Bandari hiyo wilayani Kyela mkoani Mbeya.
Mkurugenzi Mtendaji wa Songoro Marine Transport Ltd, Bw. Saleh Songoro, akionesha mchoro wa meli mbili za mizigo zenye uwezo wa kubeba tani 1000 kila moja anazoziunda kwa ajili ya matumizi katika Ziwa Nyasa, katika Bandari ya Itungi, Wilayani Kyela mkoani Mbeya, baada ya kutembelewa na ujumbe wa Serikali unaofuatilia masuala ya biashara mipakani mkoani Mbeya.


Mkurugenzi Mtendaji wa Songoro Marine Transport Ltd, Bw. Saleh Songoro, akionesha moja kati ya ya meli mbili za mizigo zenye uwezo wa kubeba tani 1000 kila moja anazoziunda kwa ajili ya matumizi katika Ziwa Nyasa, katika Bandari ya Itungi, Wilayani Kyela mkoani Mbeya, baada ya kutembelewa na ujumbe wa Serikali unaofuatilia masuala ya biashara mipakani mkoani Mbeya.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Songoro Marine Transport Ltd, Bw. Saleh Songoro, akionyesha mchoro wa meli mbili za mizigo za MV Ruvuma na Mv Njombe alizoziunda wakati Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Amina Khamis Shaaban (wa kwanza kulia), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani Balozi Hassan Simba Yahya (wa pili kulia), Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof. Adolf Mkenda (wa tatu kushoto) walipozulu Bandari ya Itungi, iliyoko Wilayani Kyela mkoani Mbeya.
Mkurugenzi Mtendaji wa Songoro Marine Transport Ltd, Bw. Saleh Songoro, akiongoza ujumbe wa Serikali kutoka Wizara za Fedha, Uwekezaji, na mambo ya Ndani kujionea kazi ya ujenzi wa Meli mbili za mizigo zenye uwezo wa kubeba tani 1000 za mizigo kila moja zinazojengwa katika Bandari ya Itungi iliyoko Wilayani Kyela mkoani Mbeya
Mkurugenzi Mtendaji wa Songoro Marine Transport Ltd, Bw. Saleh Songoro, akionesha mfumo wa kuongoza meli katika chumba cha nahodha wa meli ya Mv Njombe, huku Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biasha na Uwekezaji Prof Adolf. Mkenda, akiangalia kwa makini mfumo huo wa kisasa namna unavyofanya kazi.
Baadhi ya wajumbe wa Serikali waliofanya ziara katika Bandari ya Itungi mkoani Mbeya kujionea uundwaji wa meli mbili za mizigo wakishuka kwenye ngazi baada ya kumaliza kukagua meli ya Mv Njombe inayotengenezwa na Kampuni ya Songoro Marine Transport Ltd inayoshughulika na kutengeneza vyombo vya usafiri vya majini katika Bandari ya Itungi, Wilayani Kyela, mkoani Mbeya. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM) 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad