HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, February 22, 2017

NAIBU KATIBU MKUU- NISHATI AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KWENYE MKUTANO WA MAFUTA KONGO

 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia mbele) akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kalemie, Kongo kwa ajili  ya kushiriki mkutano  wa kubadilishana data na uzoefu kuhusu mafuta katika Tanganyika uliofanyika hivi karibuni nchini Kongo. Nchi nyingine zilizoshiriki ni pamoja na Burundi, Kongo na  Zambia. Wengine kutoka kushoto ni  Gavana wa Jimbo la  Tanganyika – Kongo, Richard Ngoy Kitangala, Waziri wa Migodi na Madini Nchini Zambia, Chris Yaluma na Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, Profesa Aime Ngoi-Mukena Lusa.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kushoto) na Gavana wa Jimbo la  Tanganyika – Kongo, Richard Ngoy Kitangala (kulia) wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, Profesa Aime Ngoi-Mukena Lusa (hayupo pichani) katika mkutano huo.
 Mkurugenzi Msaidizi wa Sheria, Wizara ya Nishati na Madini, Anna Ngowi (kushoto) pamoja na wataalam wengine kutoka Tanzania wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa katika mkutano huo.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (katikati) akiweka mchanga kwenye jiwe la msingi kuashiria uzinduzi wa ujenzi wa Chuo Kikuu cha Mafuta na Gesi katika mji wa Kalemie. Kulia kwake ni Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, Profesa Aime Ngoi-Mukena Lusa.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo ( wa pili kutoka kushoto, mbele) pamoja na viongozi wengine wakishikana mikono kama ishara ya umoja mara baada ya kuzindua ujenzi wa  Chuo Kikuu cha Mafuta na  Gesi katika mji wa Kalemie hivi karibuni .
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo ( wa tatu kutoka kushoto mbele) na Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, Profesa Aime Ngoi-Mukena Lusa ( wa sita kutoka kulia mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na watendaji  wengine mara baada ya uzinduzi wa ujenzi wa  Chuo Kikuu cha Mafuta na  Gesi katika mji wa Kalemie hivi karibuni .
 Mtaalam kutoka Idara ya Nishati, Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Athur Lyatuu (kushoto) akibadilishana mawazo na mmoja wa wajumbe wa mkutano huo.
Ujumbe kutoka Tanzania ukifuatilia hoja mbalimbali zilizokuwa zinajadiliwa katika mkutano huo.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad