HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, February 21, 2017

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM PAUL MAKONDA AMEKABIDHIWA HEKALI 1500 NA AZIMIO HOUSING ESTATE LEO

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amekabidhiwa hekali 1500 na Mkurugenzi wa Azimio Housing Estate Mohamed Iqbal kwa ajili ya viwanda vidogo.
Akizungumza mara baada ya makabidhiano hayo  eneo la Kisarawe II wilaya ya Kigamboni Mkurugenzi huyo amesema wameamua kumkabidhi eneo hilo RC Makonda kwa ajili ya kuunga mkono jitihada za Rais Magufuli za kuijenga Tanzania ya viwanda ili kuwakomboa wananchi wenye uchumi wa kati.
Kwa upande wake RC Makonda ameeleza kuwa dhamira ya viwanda ya Rais Magufuli inabidi itafsiriwe kwa vitendo, hivyo eneo hilo litatumika kwa ajili ya ufugaji, kilimo, usindikaji, utengenezaji wa sabuni na eneo hilo litatumika na wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam.
Pia RC  Makonda ameongeza kuwa Mkoa wa Dar es Salaam unajengwa na wana Dar es Salaam wenyewe hivyo kama kuna watu wanataka kujitolea kwa ajili ya maendeleo ya Dar es Salaam wafanye hivyo.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul  Makonda akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya makabidhiano hayo  eneo la Kisarawe II wilaya ya Kigamboni leo jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul  Makonda akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa leo jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul  Makonda akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa wakiangalia ramani ya eneo hilo, leo jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe: Paul Makonda  (watatu kutoka kulia)  akiwa amefuatana na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa, na Mkurugenzi wa Azimio Housing Estate,Mohamed Iqbal    wakikagua eneo hilo
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda  akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa,
Muomoneke wa  eneo hilo alilokabidhiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad