HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, February 21, 2017

MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI LA PPF WAFANYIKA MKOANI MOROGORO

Mfuko wa pensheni wa PPF ulifanya kikao cha Baraza la Wafanyakazi Mkoani Morogoro mwishoni mwa wiki. Katika kikao hicho moja ya mada iliyojadiliwa ni uwekezaji katika kilimo cha miwa na kiwanda cha sukari katika eneo la Mkulazi mkoani Morogoro ambayo iliwasilishwa na Mkurugenzi wa Muda wa Kampuni ya Mkulazi Holdings Co. Ltd, Nicander Kileo.

Uwekezaji huo unafanyika chini ya Kampuni ya Mkulazi Holdings Ltd ambayo ni Kampuni Tanzu ya Mfuko wa Pensheni wa PPF na Shirika la Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF). Uwekezaji wa kiwanda hiko cha sukari upo katika eneo lenye ukubwa wa zaidi ya hekari 63,000 na upo katika hatua za awali ambapo unatarajiwa kuzalisha tani 200,000 za sukari utakapokamilika. Mradi huo utapunguza uhaba wa sukari nchini na kutoa fursa za ajira kwa Watanzania.

Katika kikao hicho cha Baraza la Wafanyakazi wa PPF Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio alimkaribisha Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Prof. Godius Kahyarara ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Mkulazi Holdings Co. Ltd kuelezea mradi wa ubia kati ya PPF na NSSF.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa PPF (katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa baraza la wafanyakazi ambapo katika kikao hicho PPF walimkaribisha Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof. Godius Kahyarara kuelezea mradi wa ubia kati ya PPF na NSSF, katika Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa PPF kilichofanyika mkoani Morogoro mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Prof. Godius Kahyarara akitoa ufafanuzi juu ya uwekezaji katika viwanda cha Mkulazi ambapo aliwapongeza wafanyakazi wa PPF kwa kuupokea mradi huo.
Kutoka Kushoto, Mkurugenzi Mkuu Wa Mfuko Wa Pensheni Wa PPF Ndg. William Erio, Mkurugenzi wa Muda wa Kampuni ya Mkulazi Holdings Co. Ltd. Ndg. Nicander Kileo ambayo ni Kampuni Tanzu ya Mfuko wa PPF na NSSF na Mkurugenzi Wa Shirika la Taifa Wa Hifadhi Ya Jamii (NSSF) Prof. Godius Kahyarara wakijadiliana wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa PPF mwishoni mwa wiki.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad