HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, February 20, 2017

Makamba akomelea msumari wa pombe za viroba

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira , January Makamba amesema kuwa Tanzania ni nchi ambayo pombe inapatikana kirahisi.
Kauli hiyo inatokana na agizo la waziri mkuu juu ya kuzuia matumizi ya  pombe  za mifuko ya Plastiki kutokana na adhari za pombe katika jamii.
Makamba ameyasema hayo leo wakati akitangaza juu ya uzuiaji wa viroba katika mifuko ya plastiki, amesema kuwa kuanzia Machi moja ni marufuku kwa  pombe za mifuko ya plastiki ni mwisho na wataofanya biashara hiyo watachukuliwa hatua.
Amesema kuwa wanaanda kanuni ambazo zitabana biashara hiyo kutokana na kufanywa kwa muda mrefu bila serikali kupata kodi biashara ya pombe katika mifuko ya plastiki.
Makamba amesema kuwa biashara hiyo itakuwa ngumukwa watengenezaji kutokana na masharti  yaliyokuwepo kwa wale ambao wataomba biashara hiyo.
Aidha amesema  kuwa kamati za ulinzi wilaya kufanya operesheni katika maeneo yao ikiwa katika mipaka ambayo pombe za  viroba zinaweza  kuingia.
Makamba amesema kuwa pombe za viroba inatakiwa kuwa historia na kuanza kuwepo kwa pombe katika chupa za plastiki au kioo kwa milimita 250 .
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano, Januari Makamba (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa agizo la kupiga marufuku uzalishaji na uuzaji wa pombe aina ya viroba leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano Profesa Faustine Kamuzora na Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi hiyo Richard Muyungi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano, Januari Makamba (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa agizo la kupiga marufuku uzalishaji na uuzaji wa pombe aina ya viroba leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano Profesa Faustine Kamuzora na Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi hiyo Richard Muyungi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad