HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, February 10, 2017

JOHN BARNES WA LIVERPOOL KUTUA NCHINI KUANGALIA KOMBE LA STANDARD CHARTERED

  Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Baraza la Michezo nchini (BMT) Bw. Dionis Malinzi (katikati) akiwa ameambatana na Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Sanjay Rughani (kulia) pamoja na Mkuu wa Mahusiano wa Benki ya Standard Chartered, Juanita Mramba wakiwasili kwenye sherehe za uzinduzi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mahusiano wa Benki ya Standard Chartered, Juanita Mramba akizungumzia tukio adhimu la Benki ya Standard Chartered, Tanzania Limited kutimiza miaka 100 tangu ilipofungua milango yake nchini Tanzania kabla ya kumkaribisha Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo, Bw. Sanjay Rughani kutoa risala katika sherehe za uzinduzi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.
  Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Sanjay Rughani akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari wakati wa sherehe za uzinduzi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa iadara ya Fedha wa Benki ya Standard Chartered, Abdulrahman Said (wa pili kushoto) akizungumzia katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu ujio wa mchezaji aliyewika wa timu ya Liverpool, John Barnes ambapo wateja wa Benki hiyo watapata fursa ya kukutana na mchezaji huyo.
Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Baraza la Michezo nchini (BMT) Bw. Dionis Malinzi (wa pili kulia) akitoa baraka zake kwenye sherehe za uzinduzi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesiga Celestine.
 Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesiga Celestine (kulia) akitoa salamu za TFF kwenye sherehe za uzinduzi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam. 
 Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesiga Celestine (kulia) akimkabidhi bendera ya TFF Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Sanjay Rughani wakati wa sherehe za uzinduzi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Baraza la Michezo nchini (BMT) Bw. Dionis Malinzi (wa pili kulia) na Mkuu wa idara ya Fedha wa Benki ya Standard Chartered, Abdulrahman Said.
 Mkutano na waandishi wa habari ukiendelea wakati wa sherehe za uzinduzi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.
  Mchambuzi mkongwe wa kandanda nchini, Dr. Leaky Abdallah (kulia) ambaye pia ni mshabiki mkubwa wa Liverpool akitoa uchambuzi wa timu hiyo barabara ya kuelekea Anfield wakati wa sherehe za uzinduzi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.
  Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Sanjay Rughani (katikati) akimkabidhi zawadi mgeni rasmi Mwenyekiti wa Baraza la Michezo nchini (BMT) Bw. Dionis Malinzi (wa pili kulia) huku wengine wakishuhudia tukio hilo. Kulia ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesiga Celestine, Mkuu wa idara ya Fedha wa Benki ya Standard Chartered, Abdulrahman Said (kushoto) na Mchambuzi mkongwe wa kandanda nchini, Dr. Leaky Abdallah (kulia) ambaye pia ni mshabiki mkubwa wa Liverpool (wa pili kushoto).
 Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Sanjay Rughani (katikati)akimkabidhi zawadi Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesiga Celestine (kulia) kwenye sherehe za uzinduzi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.
 Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Sanjay Rughani (wa tano kulia) akimkabidhi zawadi Mchambuzi mkongwe wa kandanda nchini, Dr. Leaky Abdallah (wa tatu kushoto) ambaye pia ni mshabiki mkubwa wa Liverpool katika sherehe za uzinduzi huo. Wa pili kulia ni Mkuu wa Mahusiano wa Benki ya Standard Chartered, Juanita Mramba.
 Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Sanjay Rughani (kushoto) akibadilishana mawazo na Mchambuzi mkongwe wa kandanda nchini, Dr. Leaky Abdallah ambaye pia ni mshabiki mkubwa wa Liverpool kabla ya kuanza kwa mechi ya ufunguzi wa mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Baraza la Michezo nchini (BMT) Bw. Dionis Malinzi katika picha ya pamoja na timu A na B na waamuzi wa mechi hiyo ya ufunguzi wa wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Baraza la Michezo nchini (BMT) Bw. Dionis Malinzi akisalimiana na vikosi vya timu A na B kabla ya kuanza kwa mechi hiyo ya ufunguzi wa wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Baraza la Michezo nchini (BMT) Bw. Dionis Malinzi akibutua mpira kuashiria uzinduzi rasmi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.
 Kapteni wa timu A Majuto Omary wa gazeti la Mwananchi akiwatoka wachezaji wa timu B ikiongozwa na Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Sanjay Rughani wakati wa mechi ya ufunguzi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.
 Mpiga picha wa Azam TV akimtoka Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Sanjay Rughani wakati wa mechi ya ufunguzi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.
  Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesiga akikabidhi zawadi kwa wachezaji wa timu A baada ya kuichapa bao 1-0 timu B kwenye sherehe za uzinduzi rasmi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa Baraza la Michezo nchini (BMT) Bw. Dionis Malinzi
  Kapteni wa timu A Majuto Omary kutoka  gazeti la Mwananchi akifurahia zawadi yake baada ya timu yake kuibuka kidedea dhidi ya timu B kwa bao 1-0 wakati wa mechi ya ufunguzi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja timu A iliyoibuka kidedea dhidi ya timu B kwa bao 1-0 kwenye sherehe za uzinduzi rasmi wa awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield uliofanyika katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam. 

Na Mwandishi wetu,
MMOJA wa wachezaji waliowika na timu ya Liverpool, John Barnes atawasili nchini mwanzoni mwa mwezi Machi tayari kwa mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017 yatakayohusisha timu za eneo hili la Afrika Mashariki.
Kauli hiyo imetolewa na  Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered , Tanzania Sanjay Rughani wakati wa uzinduzi wa  awamu ya pili ya mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017, barabara ya kuelekea Anfield katika sherehe murua iliyofanyika kwenye  viwanja  vya Jakaya Kikwete Youth Park.
Katika uzinduzi huo timu mbili za wachezaji watano watano zilicheza kwa dakika kumi na mshindi alipewa zawadi.
Miongoni mwa majina muhimu waliokuwa katika timu zilizoshiriki kuzindua kombe hilo ni Majuto Omar ambaye ndiye aliyetoa pande lililotikisa wavu uliokuwa ukilindwa na kipa Edina. Wengine ni Mtendaji mkuu wa benki hiyo Sanjay Rughani na mwandishi wa Nipashe Somoe Ng'itu.
John Barnes akiwa nchini atazuru mazoezi ya timu ya Taifa ya vijana walio chini ya umri wa miaka 17 Serengeti Boys, vijana wanaotokea katika mazingira magumu au familia za kipato cha chini pamoja na watoto ambao wana akaunti katika benki ya Standard Chartered.
Taarifa zaidi katika uzinduzi zinasema kwamba Mashindano ya  kombe la Standard yanayohusisha mpira wa miguu unaochezwa kwa dakika 10, dakika 5 kila upande na yanaandaliwa kwa kushirikiana na klabu ya mpira wa miguu ya Liverpool FC ambapo safari hii ikiwa ni mara ya pili tangu yalipozinduliwa nchini  mwaka 2015 kwa mafanikio makubwa.
Standard Chartered ndio wadhamini wakuu wa klabu ya Liverpool tangu mwaka 2010 hadi 2018/2019.
Kama sehemu ya ushirikiano wake na klabu ya Liverpool, Benki ya Standard Chartered imekuwa ikipanga mashindano ya mpira wa miguu  ambayo hulenga masoko muhimu ya benki hiyo yaliyopo katika mabara ya Asia, Afrika na Mashariki ya Kati huku pia ikiyatumia kama jukwaa linaloshirikisha kikamilifu mashabiki wa soka wa maeneo hayo na pia kuchangia katika kukuza maendeleo ya soka.
Yakiwa katika mwaka wake wa sita, mashindano ya Kombe la Sndard Chartered yamekuwa yakiimarika mwaka hata mwaka na kutoa washindi kutoka pande zote za dunia. Mataifa ambayo yamenyakua kombe hilo ni pamoja na Kenya (2016), Korea Kusini (2015) Vietnam (2014), Thailand (2013) na Singapore (2012).
Mashindano haya hufanyika katika makundi matatu ambapo ni ndani ya nchi, nchi zaidi ya moja katika bara na fainali ambazo hufanyika katika uwanja wa Liverpool wa Anfield nchini Uingereza.
Mashindano haya mwaka huu nchini Tanzania yataleta pamoja timu 32 zinazohusisha wateja wa benki hiyo, vyombo vya habari na wadau wengine muhimu. Mashindano yanatazamiwa kutimua vumbi Jumamosi Februari 25 mwaka huu.
mashindano ya mwaka huu yanakwenda sanjari na tukio kubwa na adhimu la Benki ya Standard Chartered , Tanzania Limited kutimiza miaka 100 tangu ilipofungua milango yake nchini Tanzania.
Katika kuadhimisha tukio hilo adhimu Benki pia itaendelea mashindano yatakayojumuisha nchi zingine za eneo hili la Afrika Mashariki ambazo zitaibuka washindi katika nchi za Kenya na Uganda. mashindano hayo yatakayohusisha Kenya na Uganda yatafanyika nchini Jumamosi Machi 4 mwaka huu.
Mshindi wa mashindano hayo ya mwezi Machi ataiwakilisha Afrika Mashariki katika fainali zitakazofanyika katika uwanja wa Anfield ambapo jumla ya timu 10 kutoka katika maeneo mbaliumbali yaliyoko makampuni ya Standard Chartered zitamenyana kwa ajili ya kumpata bingwa atakayeondoka na Kombe la Standard Chartered kwa mwaka huu.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kwenye uzinduzi huo Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered , Sanjay Rughani alisema kuwa benki yake inaona fahari kushirikiana na klabu ya Liverpool akisistiza kwamba taasisi hizo mbili zinarandana kwa mambo mawili umakinifu na kujituma.
Aliongeza kuwa benki itafanya pia shughuli mbalimbali wakati wa mashindano kama sehemu ya kuadhimisha miaka 100 tangu ipige hodi nchini Tanzania.
"Tunapoadhimisha miaka 100 tangu tufungue milango yetu nchini Tanzania tunajisikia vizuri sana kuendesha tena mashindano kwa ajili ya Kombe la Standard Chartered.....tutakuwa pia wenyeji wa ziara ya John Barnes ambapo tutahakikisha anatoa ujuzi wake kadri atakavyoweza kwa klabu za vijana atakapokuwa hapa," Rughani alisema.
Naye Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Dionizi Malinzi aliishukuru Benki ya Standard Chartered  kwa msaada wake katika kukuza michezo nchini hususani mpira wa miguu pia aliwataka wakaoshiriki kutumia fursa hiyo inayokutanisha timu 32 za ndani na zile zitakazotoka nchi jirani katika kujenga uhusiano mwema.
Mshindi wa mashindano  yatakayohusisha timu zingine za Kenya na Uganda atapata tuzo ya safari ya kwenda Anfield.
Katika safari ya Uingereza  washiriki watakaopata nafasi watasafiri kwa ndege daraja la kawaida na malazi kwa siku tatu.

Aidha timu itapata mafunzo katika chuo cha mafunzo cha Liverpool (LFC) yatakayotolewa na wakongwe wa LFC kufanya ziara katika uwanja  wa Anfield na kufanya ziara Melwood kabla ya kuhudhuria mechi moja wapo ya klabu ya Liverpool itakayopigwa mwezi Mei mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad