Wamiliki wa mtandao wa Jamii Media na mkuregenzi wa mtandao huo Maxence Melo akizungumza na Maria Sarungi ambaye ni mdau wa masuala ya habari nje ya Mahakama kuu jijini Dar es Salaam
HUKUMU
ya kesi ya Kikatiba namba 9 ya mwaka 2016 iliyofunguliwa mwaka jana na
Kampuni ya Jamii Media ikipinga baadhi ya vifungu vya sheria ya makosa
ya mtandao kwa kile kuingilia uhuru wa maoni na kujieleza wa wananchi
imeshindwa kusoma huku kukiwa hakuna sababu zilizotajwa.
Akizungumza
leo eneo la Mahakama Kuu, jijini Dar es Salaam Wakili wa Jamii Media,
Benedict Ishebakaki Alex alisema awali walipata wito wa mahakama kuwa
hukumu ya kesi yao ilikuwa isomwe leo lakini wamefika mahakamani na
kutokuta taarifa zozote za kusomwa kwa hukumu hiyo.
"..Kama
mnavyojua leo tulikuwa tumekuja kwa ajili ya hukumu ya kesi yetu
iliyofunguliwa toka mwaka jana mwezi wa tatu kutokana na rekodi za
mahakama tuliambiwa tuje leo saa sita mchana kuja kupokea hukumu kama
mnavyojua majaji ambao walikuwa wanasikiliza kesi yetu ni majaji watatu
Mh. Jaji Koroso, Mh. Jaji Khalfan na Mh. Jaji Kitusi lakini tumefuatilia
leo hapa pamoja na mawakili wa serikali, lakini tulikuwa tunajua jaji
Koroso hayupo kuna taarifa kuwa amehamishwa...lakini tulikuwa tunajua
labda kuna rekodo yoyote kuwa labda amemwachia faili nani au hukumu
itasomwa lini tena...tunaona makarani wanasema hawana taarifa zozote juu
ya hukumu hiyo.
Wakili huyo alisema yeye
pamoja na mawakili wa Serikali wataendelea kufuatilia kujua hukumu hiyo
itasoma lini ili waweze kuipokea.
Kwa upande
wake Mwanaharakati wa haki ya kupata habari nchini, Simon Mkina,
akizungumzia kadhia ya hukumu hiyo kutoonekana, amesema inashangaza
kuona mahakama hiyohiyo iliyotoa tarehe ya kutolewa hukumu, watendaji
wake wanatupiana mpira kuhusu ilipo.
Hata
hivyo Mkina aliongeza katika mazingira ya sasa, mahakama ni mhimili
pekee unaobaki kuwa kimbilio ili kupatikana kwa haki, hivyo haipaswi
kutiliwa shaka katika utendaji wake.
Kampuni ya
Jamii Media, waendeshaji wa mitandao ya JamiiForums.com na
FikraPevu.com mwaka jana walifungua kesi ya kikatiba wakipinga baadhi ya
vifungu vya sheria ya makosa ya mtandao kwa kile kuingilia Uhuru wa
Maoni na Kujieleza wa wananchi.
Katika kesi ya
msingi iliyofunguliwa Mahakama Kuu, Kampuni ya Jamii Media ilitaka
Sheria ya Makosa ya Mtandao, kifungu cha 32 na 38 viangaliwe upya kwa
kuwa vinasababisha kuvunjwa kwa haki za msingi za Watanzania watumiao
mitandao ili kulinda maslahi ya umma kwa kuzingatia vifungu 26(2) na
30(3) vya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.
Mtandao
wa JamiiForums ni mtandao mkubwa wa Kiswahili kwa Afrika Mashariki na
Duniani ukiwa na wasomaji wasiopungua Milioni 4 kwa mwezi ambapo kwa
mwaka 2016, mtandao huu unatimiza rasmi miaka 10 tangu uanzishwe.
Mtandao huu unasifika kwa kutoa fursa ya kipekee kwa watumiaji wake
kutoa yaliyo mioyoni mwao huku wengine wakijifunza mbinu kadha wa kadha
za kijasiriamali, afya, elimu na hata kuibuka wanasiasa wapya
waliofundwa na wana JamiiForums.
Mkurugenzi wa Jamii Forum, Maxence Melo akiwa na Mmiliki Mwenza Mike Mushi wakizungumza na wakili wao, Benedict Alex Mahakama kuu jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa Jamii Forum, Maxence Melo akiwa na Mmiliki Mwenza Mike Mushi wakitoka nje ya Mahakama kuu jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa Jamii Forum, Maxence Melo akiwa na Mmiliki Mwenza Mike Mushi wakitoka nje ya Mahakama kuu jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa Jamii Media, Maxence Melo akizungumza na baadhi ya waandishi na wadau wa habari waliofika katika mahakama kuu jiji Dar es Salaam
No comments:
Post a Comment