HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, February 13, 2017

AZZAN, GWAJIMA WARIPOTI POLISI

Aliyekuwa mbunge wa Kinondoni, Idd Azzan ameripoti polisi leo asubuhi baada ya kuambiwa afanye hivyo.
Akiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam, Azzan amesema baada ya kuripoti kama alivyotakiwa ameruhusiwa na kuelezwa kuwa aende katika kituo hicho baadaye.
Azzan amesema tangu watu waanze kumzungumzia kuhusiana na dawa za kulevya ni muda mrefu na hivyo amezungukwa na maadui wengi.
"Mimi tangu nianze kuzungumzwa sijaanza leo, wanasikiliza kwenye mitandao ya kijamii, hawajui mimi nina maadui wangapi ambao wananizunguka. Utakuta mtu tu ananitaja kwa chuki zake," amesema Azzan.
Amesema polisi walienda nyumbani kwake kupekuwa na hawakupata kitu chochote. “Nasubiri hiyo baadaye wataniambia kitu gani”
Wakati huo huo, Mchungaji Josephat Gwajima aliyedai angekwenda kuwaona wenzake waliosalia polisi, naye pia ameripoti polisi saa 10.46 asubuhi
Msaidizi wa askofu huyo amesema Gwajima ametakiwa kuripoti tena mchana huu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad