HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, February 10, 2017

AZAM YATIA KAMBI MKOA WA PWANI TAYARI KUWAVAA RUVU SHOOTING



Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii



Timu ya Azam FC, imetia nanga mkoani Pwani, tayari kabisa kwa ajili ya mchezo wa kesho wapinzani wao Ruvu Shooting utakaofanyika kesho katika Uwanja wa Mabatini mkoani humo.


Mchezo huo nunaotarajiwa kupigwa majira ya saa 10 Alasiri utakuwa wanushindani mkubwa sana hasa baada ya Azam kukumbuka sare ya mechi ya awali iliyomalizika kwa goli 2-2.

Kikosi cha Azam FC kimeondoka jana kikiwa na morali kubwa ya kufanya vizuri kwenye mchezo huo kutokana na mazoezi makali wanayopewa chini ya benchi la ufundi linaloongozwa na Mromania, Aristica Cioaba, Msaidizi wake, Idd Cheche na Kocha Makipa, Idd Abubakar.


Akizungumza kuelekea mchezo huo, Kocha Msaidizi wa Azam FC, Idd Nassor Cheche, amesema kuwa wanakwenda huko kuendeleza wimbi lao la ushindi kwa kuichapa Ruvu Shooting.

“Tunawaheshimu wapinzani wetu, tunajua upinzani wanaotuonyeshaga kila tunapokutana, lakini tumejipanga kufanya vizuri, rungu lililotumika kuua tembo ndilo litakalotumika kuua sisimizi, tunawaomba mashabiki wetu wasubirie kufurahi,” alisema.

Hadi hivi sasa Azam FC imefanikiwa kujikusanyia jumla ya pointi 37 katika nafsi ya tatu kwenye msimamo ikilingana kwa pointi na Kagera Sugar iliyochini yake, inazidiwa pointi 12 na kinara Yanga aliyejikusanyia 49 na Simba iliyonafasi ya pili nazo 48.

Msafara wa Azam FC umeondoka na jumla ya wachezaji 21, ambao ni makipa Aishi Manula, Mwadini Ally, Metacha Mnata, mabeki ni Aggrey Morris, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, Yakubu Mohammed, Bruce Kangwa, Gadiel Michael, Ismail Gambo, Abdallah Kheri. 

Viungo ni Nahodha Msaidizi Himid Mao, Frank Domayo, Mudathir Yahya, Masoud Abdallah, mawinga Joseph Mahundi, Khamis Mcha, Ramadhan Singano na washambuliaji Yahaya Mohammed, Samuel Afful na Shaaban Idd.

Wachezaji wengine waliobakia wameachwa kwa sababu mbalimbali, nahodha John Bocco, Salum Abubakar, Stephan Kingue, Daniel Amoah, wakiwa ni wagonjwa, huku winga Enock Atta Agyei kibali chake cha uhamisho kikiwa bado hakijawasili nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad