HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, January 17, 2017

Kliniki ya Airtel Rising Stars yaanza Dar

Mkurugenzi wa Ufundi wa Soka la vijana TFF, Kim Paulsen akitoa maelekezo kwa wachezaji wa timu ya vijana U-17 wakati wa ufunguzi wa kliniki ya Airtel Rising Stars katika uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam jana.

Kliniki ya Soka ya Airtel Rising Stars imeanza leo kwenye Uwanja wa Karume kwa kuwakutanisha wavulana 40 na huku ya wasichana ikifanyika kwenye uwanja wa JK Park zamani kidongo chekundu.

Akizungumza wakati wa kliniki hiyo, Kocha Mkuu wa Timu ya Serengeti Boys, Bakari Shime alisema, ‘kwanza tutakuwa tukiangalia ufundi binafsi wa mchezaji’. Hii ni mara ya kwanza kukutana na wachezaji hawa na kuangalia vitu binfasi ambavyo mchezaji anatakiwa kuwa navyo hii itatusaidia kujua ni sehemu ipi ya kutilia mkazo.

 Juhudi binafsi za Mchezaji, Ufundi na stamina (ukakamavu) ni vitu muhimu kwa mchezaji kuwa navyo katika kiliniki hii, hiyo ndio sababu leo kwa siku ya kwanza wachezaji tumewapa nafasi ya kuchezea mpira ili kuangalia vitu hivyo,’ alisema Shime.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa kliniki ya Airtel Rising Stars kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam jana.

Lakini pia tutapata nafasi ya kuingalia timu yetu ye Serengeti Boys kama ina mapungufu yoyote na kama kutakuwa na wachezaji wenye umri mkubwa basi hauwaruhusiwa  kuendelea kuchezea timu ya vijana.

 Hapa ndipo tutapa fursa ya wachezaji wa kuweza kuziba nafasi zilizoachwa wazi katika timu hiyo,  Kwa wiki hii yote tutakuwa na kazi ya kushirikiana na Makocha wengine  kuikamilisha zoezi hili, aliongeza Shime.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Maendeleo ya Soka la vijana TF,  Ayoub Nyenzi alisema, ‘klikini ya Airtel Rising Stars inatoa fursa pana kwa vijana chipukizi kuonyesha uwezo wao mbele ya makocha wenye uzoefu wa mpira wa miguu nchini’. 
Katibu Mkuu TFF, Selestine Mwesigwa akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa kliniki ya Airtel Rising Stars kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam jana.
Hii ni nafasi adhimu kwa  vijana wetu kuendelea kuonyesha uwezo wao na kuzidi kuendeleza vipaji vyao. Sio lazima wachezaji wote hawa hawawezi kuchanguliwa kuchezea timu ya vijana ya Serengeti Boys, lakini kuna klabu zetu ambazo zinaitahitaji wachezaji kwenye timu zao za vijana. Hii ndio nafasi kwao kujitokeza na kuangalia wachezaji wenye uwezo wa kuchezea timu zao,  Ayoub aliyasema hayo jana.

Naye Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania, Beatrice Singano Mallya alisema, ‘kufanyika kwa kliniki ya Airtel Rising Stars kunahitimisha awamu ya sita ya michuano ya Airtel Rising Stars’  ambayo ilifanyika kwa Mikoa tisa nchini kwa mafanikio makubwa sana. 
‘Nachukua fursa hii kuwashukuru TFF pamoja na wadau wote wa mpira wa miguu nchini ambao tumeshirikiana kwenye 2016 Airtel Rising Stars. Michuano hii lifanyika kwa mafanikio makubwa sana na leo tunapaonza kliniki hii inayojumuisha wachezaji bora naomba tuendelea tushirikiana kwa pamoja ili vijana wetu waweze kutimiza ndoto zao za kuwa wachezaji bora katika maisha yao’ alisema Mallya

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad