HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, November 1, 2016

WAJASILIRIAMALI PWANI WATAKIWA KUWA WABUNIFU

NA VICTOR MASANGU, BAGAMOYO 

WAJASIRIAMALI nchini wametakiwa kuhakikisha wanakuwa wabunifu na kutengeneza bidhaa zenye ubora wa kiwango cha juu ili kuweza kuleta ushindani na kuzipeleka katika soko la afrika mashariki ambalo lina idadi kubwa ya watu ili ziweze kuuzika na kukuza pato la Taifa.

Kauli hiyo imetolewa na MKUU wa Mkoa wa Pwani Injnia Evarist Ndikilo wakati wa sherehe za ufungaji wa maonyesho ya 9 ya wajasiriamali wadogo wadogo kutoka kanda ya mashariki yaliyofanyika katika viwanja vya Mwanakalenge Wilayani Bagamoyo.

Ndikilo alisema kwamba ili bidhaa zinazotengenezwa na wajasiriamali wa Tannzania ziweze kuuzika katika soka la afrika mashariki kunahitajika juhudi za makusudi kutoka kw amamalaka ya chakula na dawa (TFDA) pamoja na Shirika la viwango Tanzania (TBS) kuzingatia maagizo waliyopatiwa na serikali wakati wa ufunguzi wa maonyesho hayo ili kuweza kukuza uchumi wa nchi.

Ndikilo akizungumzia kuhusina na changamoto inayowakabili wajasiriamali hao katika suala la upatikanaji wa vifungashio katika kuhifadhi bidhaa zao amesema kwamba serikali ya awamu ya tano kupitia Wizara ya viwanda na biashara ipo tayari kutoa fungu la fedha kwa ajili ya kuweza kuwa na vifungashio hapa nchini kuliko kuviagizia kutoka nje ya nchi kwani ni gharama kubwa.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo akiwahutubia wajasiriamali hawapo pichani wakati wa sherehe za ufungaji wa maonyesho ya tisa kanda ya mashariki yaliyofanyika katika viwanja vya mwanakalenge Wilayani Bagamoyo.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
mmoja wa wajasiriamali walioshiriki katika maonyesho ya tisa ya kanda ya mashariki yaliyofanyika katika viwanja vya mwanakalenge Wilayani Bgamoyo Jacob Luis akiwa katika gari yake ambayo ameitengeneza yeye mwenyewe ambapo mpaka kukamilika kwake ametumia gharama ya kiasi cha shilingi milioni tisa(PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad