HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 7, 2016

Serikali yapongezwa na Hakielimu.

Mkurugenzi Mtendaji  wa Hakielimu, John Kalage, akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya hatua zilizo chukuliwa na Serikali kwa Walimu wa Mbeya Day.

Na Humphrey Shao, Blog ya Jamii.
TAASISI isiyo ya kiserikali inayosimamia mwenendo wa Elimu hapa nchini ya Hakielimu imeipongeza Serikali kwa hatua za kinidhamu zilichokuliwa kwa wale wote waliohusika kutoa adhabu ya kikatili kwa mwanafunzi wa kidato cha 3 ,Sebastian Chinguku wa shule ya sekondari ya Mbeya day.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo jijini Dare s Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa wa tasisi hiyo, John Kalage amesema kuwa  wamepokea tarifa hiyo kwa masikitiko makubwa sana mara baada ya kuona ukatili uliopotiliza.

“tunaipongeza Serikali kwa kuchukua hatua za awali zikiwemo kuliagiza Jeshi la Polisi nchini kuchukua hatua za haraka dhidi ya wanafunzi waliokuwa wanafanya mazoezi ya kufundisha waliohusika katika tukio lile. Aidha tunampongeza Mwalimu aliyethubutu kukemea na kufichua ukatili huu uliopotiliza hivyo tunaomba mamlaka husika zichukue hatua madhubuti za kulinda uhai hata ajira ya mwalimu huyu jasiri” amesema Kalage.

Ameongeza kuwa Hakielimu inaitaka Serikali kuhakikisha suala hili linashughulikiwa kwa upana wake na kuendelea kuitaharifu jamii juu ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya waliohusika na ukatili huu.

Alimaliza kwa kusema kuwa licha ya tukio la Mbeya linaonekana kuchukua mjadala mpana hapa nchini kwa sasa, tunapenda kuitaharifu serikali kuwa matukio ya ukatili dhidi ya watoto wa mwaka 2011 imeonesha kuwa kuna ukatili wa kutisha sana kwa watoto katika shule nyingi hapa nchini vikiwemo vya kimwili na kingono.

Aliweka wazi kuwa adhabu kama hizi zinapotolewa kwa watoto, husababisha wato kutafuta namna ya kukwepa adhabu hiyoo na kupelekea kukimbia masomo yao na hatimaye kuacha shule kabisa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad