HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, October 31, 2016

Kitabu kinachoelezea mbinu zinazotumiwa na watu matajiri kufanikiwa kimaisha chazinduliwa Dar

Imeelezwa kwamba watu wengi wamekuwa wakishindwa kufanikiwa kimaisha kutokana na kutokuwa na mipango ya kimaisha ambayo wanaweza kuifanyia kazi ili waweze kufanikiwa kama jinsi ilivyo kwa baadhi ya watu ambao wanaonekana kuwa na mafanikio.

Hayo yamesemwa na Mwandishi wa kitabu cha TIMIZA MALENGO YAKO, Joel Nanauka wakati wa uzinduzi wa kitabu hcho ambacho kinnaelezea mbinu 60 ambazo zinatumiwa na watu waliofanikiwa kimaisha kuweza kufikia alengo ambayo wamejiwekeakatika maisha yao.

Nanauka alisema watu wengi wamekuwa wakitamani kufanikiwa lakini wamekuwa hawajui ni hatua gani za kupitia na kufanikiwa na baada ya yeye kufanya utafiti wa muda mrefu kwa watu mbalimbali duniani waliofanikiwa na wasiofanikiwa, ameweza kupata mbinu 60 ambazo ndiyo zinatofautisha watu wa matabaka hayo mawili.
Alisema kupitia kitabu hicho msmaji ataweza kufahamu ni mambo gani anatakiwa kufanya na yapi hatakiwi kufanya ili kufanikiwa kama wengine kwa kuzingatia mbinu ambazo pia zimekuwa zikitumiwa na watu waliofanikiwa katika nyanja mbalimbali kama biashara, michezo, sanaa na hata uongozi.

"Watu wengi wanapenda kufanikiwa lakini kama huna malengo huwezi kufanikiwa, watu wengi hawajui wanatumia njia gani ili kufanikiwa na hadi wanaondoka duniani wanaondoka na ndoto walizokuwa nazo, ndoto ambazo zilitakiwa kubaki zikifanya kazi duniani,

"Sababu ya kuandika kitabu hiki ilianza nipotaka kujua utofauti wa waliofanikiwa na wasiofanikiwa, aliyefanikiwa kwa aliye Marekani na Tanzania na asiefanikiwa aliye Tanzania a Mareani, nilianza kusoa kwanini wengine wanaweza kufanikiwa katikati ya mamilioni ya watu na baada ya kupata mawazo ya jumla ndiyo nikapata mbinu 60 ambazo zipo katika kitabu cha TIMIZA AHADI YAKO," alisema Nanauka.

Nanauka alisema kitabu hicho kitakuwa kikuzwa kwa Tsh. 10,000 na anaamini kila ambaye ataweza kusoma kitabu hicho ataweza kupata kitu kipya ambacho kitaweza kumsadiakufanikiwa na kufika ndoto abazo anatamani kuzifikia.

"Matumaini yangu kila atakaesoma kitabu hiki maisha yake yabadilike kutokana na mambo ambayo atayasoma na kila mtu hatajutia kusoma kitabu hiki, nimekiandaa kwa muda mrefu kwa kufanya tafiti nyingi na kuweka mifano ambayo naamini itabadili maisha ya watu wengi wataokisoma," alisema Nanauka.

Mwandishi wa kitabu cha TIMIZA MALENGO YAKO, Joel Nanauka akizungumza kuhusu kitabu cha TIMIZA ALENGO YAKO na jinsi ambavyo kinaweza kubadili maisha ya watu ambao watakisoma.

Mwandishi wa kitabu cha TIMIZA MALENGO YAKO, Joel Nanauka akizunguza kuhusu kitabu cha TIMIZA AHADI YAKO wakati wa uzinduzi wa kitabu hicho ambacho kitauzwa kwa Tsh. 10,000.

Mshauri wa Saikolojia na Mahusiano, ambaye pia ni Mhadhiri wa somo la Saikolojia katika Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Dr. Chris Mauki akizungumza mambo ya kuzingatiwa ili mtu afanikiwa kimaisha.

Mshauri wa Saikolojia na Mahusiano, ambaye pia ni Mhadhiri wa somo la Saikolojia katika Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Dr. Chris Mauki akifanya uzinduzi wa kitabu cha TIMIZA AHADI YAKO.

Mwandishi wa kitabu cha TIMIZA MALENGO YAKO, Joel Nanauka akipiga makofi mara baada ya Mshauri wa Saikolojia na Mahusiano, ambaye pia ni Mhadhiri wa somo la Saikolojia katika Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Dr. Chris Mauki kukamilisha zoezi la uzinduzi wa kitabu hicho.

Makamu wa Rais wa TCCIA, Octavian Mshiu akilezea jinsi kitabu TIMIZA MALENGO YAKO kilivyoandaliwa na faida kwa msomaji.

Baadhi ya watu waliohudhuria uzinduzi wa kitabu cha TIMIZA MALENGO YAKO.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad