HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, October 20, 2016

BARAZA LA TAIFA LA USALAMA BARABARANI LAKUTANA KUJADILI MAENDELEO YA MKAKATI WA KUPUNGUZA AJALI

Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na wajumbe wa baraza hilo wakati wa kikao cha kujadili maendeleo ya Mkakati wa Kupunguza Ajali za Barabarani. Kulia ni Katibu Mtendaji wa baraza ambaye pia ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga.Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa wizara hiyo, Dar es Salaam.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani nchini ambaye pia ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, akifungua kikao cha kujadili maendeleo ya Mkakati wa Kupunguza Ajali za Barabarani.Kushoto ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa wizara hiyo, Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akiongoza kikao cha kujadili maendeleo ya Mkakati wa Kupunguza Ajali za Barabarani. Kushoto ni Katibu Mtendaji wa baraza ambaye pia ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Mohamed Mpinga.Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa wizara hiyo, Dar es Salaam.
Mjumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani kutoka Kikosi cha Usalama Barabarani, Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Polisi, Mossi Ndozero, akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya Mkakati wa Kupunguza Ajali za Barabarani kwa Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani), wakati wa kikao cha kujadili maendeleo ya mkakati huo, kilichofanyika katika ukumbi wa wizara, Dar es Salaam.

Mjumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Hamza Kasongo(kulia), akichangia mada wakati wa kujadili taarifa ya maendeleo ya Mkakati wa Kupunguza Ajali za Barabarani wakati wa kikao cha kujadili maendeleo ya mkakati huo.Kushoto ni mjumbe wa baraza hilo Henry Bantu. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa wizara, Dar es Salaam. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad