Jaji
Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman akisisitiza jambo kwa
waandishi wa habari walioshiriki katika Mkutano huo, miongoni mwa mambo
aliongelea ni pamoja na uzinduzi rasmi wa Mradi wa Maboresho wa huduma
utakaotekelezwa kwa kushirikiana na Benki ya Dunia (WB).
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman , akionesha nakala ya kitabu cha Mpango Mkakati wa miaka mitano (5) wa Mahakama ya Tanzania, alipokuwa katika Mkutano kati yake na Waandishi wa Habari uliofanyika mapema leo katika Ofisi za Mahakama ya Rufani (T), lengo la Mkutano huo lilikuwa ni kutoa taarifa juu ya uzinduzi rasmi wa Mpango huo utakaofanywa na Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Kassim M. Majaliwa kwa niaba ya Mhe. Rais, mnamo tarehe 21.09.2016, katika jengo jipya la Mahakama ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani. Kushoto ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali, kulia ni Mhe. Katarina Revocati, Msajili Mkuu, Mahakama ya Tanzania.
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakiwa kazini.
(Picha na Mahakama ya Tanzania)
No comments:
Post a Comment