HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 7, 2016

TSSA YATOA TAARIFA KWA SERIKALI JUU UKUZAJI UCHUMI NA UJEZI WA VIWANDA NCHINI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Viajana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama akizungumza wakati wa Mkutano wa kupokea taarifa ya Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi za Jamii nchini (TSSA), juu ya hatua iliyofikiwa na Mifuko hiyo katika ukuzaji Uchumi na ujenzi wa Viwanda nchini, uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa LAPF Mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi za Jamii nchini (TSSA), Meshach Bandawe akizungumza  wakati wa Mkutano wa kutoa taarifa kwa Serikali  juu ya hatua iliyofikiwa na Shirikisho hilo katika ukuzaji Uchumi na ujenzi wa Viwanda nchini, uliofanyika Mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof. Godius Kahyarara ambaye pia ni Mjumbe wa Shirikisho hilo, akichangia mada katika Mkutano wa kupokea taarifa ya Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi za Jamii nchini (TSSA), juu ya hatua iliyofikiwa na Mifuko hiyo katika ukuzaji Uchumi na ujenzi wa Viwanda nchini, uliofanyika Mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii (SSRA), Irene Isaka akizungumza wakati Mkutano huo uliotoa taarifa kwa Serikali  juu ya hatua iliyofikiwa na Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi za Jamii nchini (TSSA) katika ukuzaji Uchumi na ujenzi wa Viwanda nchini, uliofanyika Mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage akisisitiza jambo kwa wajumbe wa Mkutano huo uliotoa taarifa ya Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi za Jamii nchini (TSSA), juu ya hatua iliyofikiwa na Mifuko hiyo katika ukuzaji Uchumi na ujenzi wa Viwanda nchini, uliofanyika Mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Mwenyekiti wa Shirikisho hilo ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa LAPF, Eliud Sanga.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala pamoja na Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mhe. William Ole Nasha wakifatilia kwa makini taarifa hiyo iliyokuwa ikitolewa na Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi za Jamii nchini (TSSA), juu ya hatua iliyofikiwa na Mifuko hiyo katika ukuzaji Uchumi na ujenzi wa Viwanda nchini.
Katibu Mkuu ofisi ya Waziri wa Nchi, katika Ofisi ya Waziri Mkuu,
Sera, Bunge, Kazi, Viajana, Ajira na Walemavu, Eric Shitindi (kulia) akiwa na  Mwenyekiti wa Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi za Jamii nchini (TSSA) ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa LAPF, Eliud Sanga wakifatilia Mkutano huo.
Wajumbe wa Mkutano huo kati ya Serikali na Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi za Jamii nchini (TSSA).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad