HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, September 12, 2016

'TASWE - SACCOSS' WASHEHEREKEA MIAKA MIWILI TANGU KUANZISHWA KWAKE JIJINI DAR.




 
Rais wa Chama cha wenye viwanda Biashara na Kilimo nchini (TCCIA), John Mayanja atembelea baadhi ya kazi za wanawake wajasiliamali katika hafla ya Dinner Paty Gala iliyoambatana na Kusheherekea miaka miwili ya Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss) jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss), Anna Matinde akizungumza katika hafla ya kutimiza Miaka miwili ya TASWE-Saccos jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. 

Alisema kuwa TASWE ipo mikoa Tofautitofauti hapa nchini Lengo kuu la hafla ya Dinner Part Gala ni kuwafikia wanawake wengi zaidi ili kutatua changamaoto zinazowakabiri hasa kwa upande wa kipato cha mwanamke.

Alisema kuwa TASWE inamatawi 14, katika matawi hayo wameona watoe elimu ya Ujasiliamali kwa wanawake wengi zaidi hapa nchini ili kupunguza ongezeko la utegemezi na waweze kuwa wanawake wajasili na wenye nguvu.
 Mshereheshaji, Angela Bondo akizungumza katika sherehe ya kutimiza miaka miwili ya TASWE jijini Dar es  Salaam mwishoni mwa wiki.
 Rais wa Chama cha wenye viwanda Biashara na Kilimo nchini (TCCIA), John Mayanja akizungumza wakati wa kuadhimisha miaka miwili ya Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss) jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na kuwataka wanawake watumie fursa zinazojitokeza hasa kwa wale wanaotaka kusindika juisi za matunda hapa nchini kwa kuwa kuna matunda mbalimbali inapofikia msimu wake huharibika na kutupwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Plc, Ineke Bussemaker, akizungumza na wanawake wakati wa kusheherekea Miaka miwili ya Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss) tangu kuazishwa kwake na kuwa na wanachama wanawake wengi katika mikoa tofauti tofauti zaidi ya 10 hapa nchini. Alisema kuwa Wanawake milango imefunguka kwa benki hiyo hasa wakijiunga kwa makundi ili kupata mikopo yenye riba ya chini katika benki ya NMB hapa nchini.
Mtoa Maada wakati wa Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss) ikisherekea Miaka miwili jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.


 Wanawake wakiserebuka wakati wa kusherekea miaka miwili ya Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss) jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Baadhi ya wanawake waliohudhulia katika Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss)Dinner Party Gala na kusheherekea pamoja kutimiza Miaka miwili ya Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss) jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss), Anna Matinde na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Plc, Ineke Bussemaker wakimsikiliza mtoa maada wakati wa Dinner Paty Gala na kusheherekea miaka miaka miwili ya Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE) jijini Dar es Salaam.
 Burudani ikiendelea.








 Washiriki wakiwa katika hafla ya Dinner Paty Gala pamoja na Kusheherekea Miaka miwili ya Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss),jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad