Balozi wa Tamasha la Majimaji Selebuka, Nathan Mpangala ambaye pia ni mchora vibonzo akitoa mrejesho kuhusu tamasha la Majimaji Selebuka katika mkutano wa wadau uliofanyika mwishoni mwa wiki uliofanyika katika ukumbi wa ‘Nafasi Art Space’ uliopo Mikocheni, jijini Dar es Salaam. Tamasha la Majimaji Selebuka lilifanyika Songea, mkoani Ruvuma mwishoni wa mwezi wa tano mwaka huu.
Baadhi ya wadau waliojitokeza kwenye mkutano wa mrejesho kuhusiana na tamasha la Selebuka wakifuatilia makala ya video iliyokuwa ikionesha matukio mbalimbali kuhusiana na tamasha hilo.
Balozi wa Tamasha la Majimaji Selebuka, Nathan Mpangala (aliyenyoosha mkono) akifafanua jambo kwa wadau hao. Balozi huyo amewashukuru watu wote waliojitokeza na kuchangia maoni.
No comments:
Post a Comment