Katibu Mkuu wa Yanga Baraka Deusdedit.
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
TIMU ya Yanga inatarajia kucheza mchezo wa kirafiki na Mtibwa Sugar Agosti 08 ikiwa ni maandalizi ya kuendelea mchezo wao wa kimataifa dhidi ya Mo bejaia unaotarajiwa kupigwa Agosti 13 Jijini Dar es salaam.
Akizungumza na Mtandao huu, Katibu Mkuu wa Yanga Baraka Deusdedit amesema kuwa mechi hiyo itatumika kwa ajili ya kukiangalia kikosi kabla ya kuelekea mchezo wao wa kimataifa wa kombe la Shirikisho ambapo wana nafasi ndogo sana ya kufuzu ila bado hawajakata tama kwani kama wakifanikiwa kushinda michezo ilioyobaki pia inakuwa ni moja ya nafasi nzuri watakayokuwa nayo katika kundi A.
Deusdedit amesema kuwa, kwa sasa wachezaji wanaendelea na mazoezi katika viwanja vya Gymkhana na wachezaji wote wako vizuri isipokuwa Geofrey Mwashiuya ambaye bado ana P.O.P ila wengine wameanza mazoezi ua pamoja.
Mbali na hilo pia katika siku hiyo hiyo, Uongozi wa Yanga umetangaza kuitisha mkutano mkuu wa wanachama watakaojadili masuala ya ndani ya klabu yao pamoja na maendeleo kwa ujumla kuelekea ligi kuu na nini cha kufanya ambapo unatarajiwa kuanza majira ya saa 3 asubuhi katika ukumbi wa Diamond Jubilee na baadae watajumuika pamoja Uwanja wa Taifa kushuhudia mtanange huo wa kirafiki.


No comments:
Post a Comment