HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, August 15, 2016

MKIBIZA UPEPO USAIN BOLT ASHINDA MEDALI YA DHAHABU HUKO RIO

Asubuhi ya kuamkia leo huko Rio De Janeiro nchini Brazil katika michuano ya Olympic, mwanariadha Mjamaica, Usain Bolt ameweza kupata ushindi tena wa pekee kwa kujipatia medali ya dhahabu kwa kukimbia mbio za mita 100 kwa sekunde 9.81.

Bolt ameweza kumpiku mpinzani wake Justin Gatlin mwenye asili ya America ambaye yeye amekimbia kwa sekunde 9.89 na kunyakua  medali ya Silver na mshindi wa tatu Andre de Grasse mwenye asili ya Canada akikimbia kwa sekunde 9.91.

Akiwa amejizatiti kuendelea kuweka rekodi, Bolt amebakisha michezo miwili ya mwisho ambayo atakimbia siku ya jumapili na kuweza kumaliza mashindano yake ya Olympic mwaka 2016
Mwaka 2012 katika michuano ya Olympic iliyofanyika nchini London katika mbio za Mita 100 na Mita 200 aliweza kushinda zote na kuondoka na Medali za dhahabu na Olympic ya mwaka 2008 iliyofanyika Beijing katika mfululizo huo huo wa mbio za mita 100 na 200 alifanikiwa kuchukua tena medali ya dhahabu.

Mkimbiza upepo huyo tangu aanze kushiriki Michuano ya Olympic mwaka 2008 hajawahi kushinda medali tofauti na dhahabu

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad